11.1.2 Uainishaji wa kuvuja damu baada ya kuzaa

Kuvuja damu huainishwa kulingana na wakati wa kuvuja damu baada ya mtoto kuzaliwa, na kisababishi cha kuvuja kwenyewe.

Uainishaji kulingana na wakati wa kuvuja damu:

  • Kuvuja damu kwa baada ya kuzaa kwa kiwango cha kimsingi ni hali ya kuvuja damu kupita kiasi inayotokea katika awamu ya tatu ya leba au katika saa 24 baada ya kuzaa.
  • Kuvuja damu kwa baada ya kuzaa kwa kiwango cha upili (pia huitwa kuvuja damu kwa baada ya mtoto kuzaliwa) hujumuisha kuvuja damu kupita kiasi kwa kati ya saa 24 baada ya mtoto kuzaliwa na wiki 6 baadaye.

Uainishaji kulingana na kisababishi cha kuvuja hujulikana kama hali inayohusiana na mikazo au inayohusiana na jeraha. Tutajadili kuhusu kila aina na jinsi ya kuidhibiti katika somo linalofuata.

11.1.1 Ni kiwango gani cha kuvuja damu kilicho cha “kupita kiasi”?

11.2 Kuvuja damu baada ya kuzaa kunakohusiana na mikazo