11.2 Kuvuja damu baada ya kuzaa kunakohusiana na mikazo

Neno "kutojikaza" linamaanisha "ukosefu wa mikazo ya kimisuli au uwezo wa kujikaza". Kuvuja damu baada ya kuzaa kunakohusiana na mikazo hutambulika kwa kuvuja damu kupita kiasi kufuatia uterasi kukosa kujikaza vyema baada ya kuzaa, na kuwa laini, legevu na iliyokosa mikazo ya misuli.

Kwa ufasaha zaidi, katika hali ya kuvuja damu inayohusiana na mikazo, miometriamu haiwezi kujikaza na kuifinya mishipa ya damu ya mama iliyoraruka baada ya plasenta kutengana na pembezo za uterasi. (Miometriamu ni pembezo ya uterasi iliyoundwa kwa misuli.) Mara nyingi kuvuja damu baada ya kuzaa hutokea kwenye sehemu ambapo plasenta ilikuwa imejibandika hapo awali. Ikiwa miometriamu haitajikaza kwa nguvu, haitaweza kuifinya mishipa ya damu ili kudhibiti kuvuja damu.

11.1.2 Uainishaji wa kuvuja damu baada ya kuzaa

11.2.1 Visababishi vya kuvuja damu kunakohusiana na mikazo