11.3 Kuvuja damu baada ya kuzaa kunakohusiana na jeraha

Katika kuvuja damu baada ya kuzaa kunakohusiana na jeraha, kuvuja damu kupita kiasi hutokea kufuatia jeraha kwenye njia ya uzazi baada ya mtoto kuzaliwa. Jeraha linaweza kutokea kwenye seviksi, uke, periniamu, au kinyeo. Jeraha pia linaweza kuwa kupasuka kwa uterasi (Kipindi cha 10). Dalili za hali ya kuvuja damu baada ya kuzaa inayohusiana na jeraha ni damu inayovujia ukeni lakini uterasi imejikaza vyema (ni ngumu).

Jeraha kwenye mfumo wa uzazi linaweza kuzuilika. Ujuzi na udhibiti taratibu uhitajika wakati wa kuzalisha. Ikiwa leba imedumu kwa muda mrefu au fetasi imetanguliza vibaya au iko katika hali mbovu, pendekeza rufaa haraka iwezekanavyo (Kipindi cha 8).

11.2.1 Visababishi vya kuvuja damu kunakohusiana na mikazo

11.4 Punguza hatari ya kuvuja damu baada ya kuzaa