11.4.1 Hatua za dharura katika utunzaji wa waakati wa ujauzito

Wapangie wanawake walio na vipengele hatari vinavyojulikana (kama ilivyoelezwa katika hali ya kuvuja damu baada ya kuzaa inayohusiana na mikazo ya uterasi) wazalie kituoni cha afya. Humo kituoni, hatari ya kuvuja damu baada ya kuzaa inaweza kudhibitiwa kwa urahisi. Ikiwa kuvuja kutatokea, hatua ya dharura inaweza kuchukuliwa. Katika matukio ya privia ya plasenta, hali mbovu ya fetasi, au mapacha, upasuaji unaweza kuhitajika. Baadhi ya wanawake wanaweza kuwa hawataki kwenda kwenye kituo cha afya. Hata hivyo, unapaswa kuwafafanulia kwa ufasaha na kwa umakinifu kina mama walio hatarini zaidi kwa nini kuzalia nyumbani si salama. Ikiwa watakataa, hakikisha kuwa mpango ya rufaa uko tayari. Hakikisha kuwa umewatayarisha watu wa kumtolea mwanamke damu ikiwa ataihitaji.

Hatari kubwa ya kuvuja damu baada ya kuzaa inayohusiana na anemia ni mojawapo ya sababu ya umuhimu wa kuchunguza anemia kila unapotoa huduma ya wajawazito (na baada ya kuzaa). Chukua hatua kuzuia anemia.

  • Utafanya nini ili kuzuia anemia katika wanawake wajawazito unaowahudumia?

  • Washauri kuhusu lishe bora. Zingatia kuhusu chakula kinachopatikana chenye wingi wa madini ya chuma na foleti (kama vile mboga mbichi, nafaka nzima, nyama nyekundu, na mayai). Wape virutubishi mbadala ya chuma/foleti.

    Ulijifunza kuhusu mambo haya katika Moduli ya Utunzaji wa Wakati wa Ujauzito kama kitengo cha utunzaji maalum wa kabla ya kuzaa (Kipindi cha 13), lishe katika ujauzito (Kipindi cha 14), na ukingaji na matibabu ya anemia (Kipindi cha 18).

    Mwisho wa jibu

  • Utachukua hatua gani ili kuzuia anaemia inayosababiswa na malaria na mnyoo?

  • Wahimize wanawake kutumia neti iliyotiwa dawa ili wajikinge dhidi ya mbu wanaoambukiza viini vya malaria. Wape wananwake dawa (mebendazole) baada ya kipindi cha kwanza cha ujauzito iwapo wanaishi katika maeneo yenye mnyoo.

    Mnyoo na ugonjwa wa malaria umeelezwa kwa kina katika Moduli ya Magonjwa ya Kuambukiza.

    Mwisho wa jibu

11.4 Punguza hatari ya kuvuja damu baada ya kuzaa

11.4.2 Hatua za dharura katika awamu ya pili ya leba