11.4.2 Hatua za dharura katika awamu ya pili ya leba

  • Tumia pathograpu kufuatilia na kudhibiti leba na kuzuia leba kuchukua muda mrefu (Kipindi cha 4).
  • Mhimize mwanamke ahakikishe kuwa kibofu chake ni kitupu.
  • Usimkubalie mama kusukuma mtoto kabla ya seviksi kupanuka vyema.
  • Usifinye juu ya uterasi (shinikizo la fandasi) ili kusaidia kuzaliwa kwa mtoto.
  • Msaidie mwanamke kuzaa kwa kudhibiti kichwa na mabega ya mtoto ili kuzuia majeraha (Kipindi cha 3). Weka vidole vya mkono wako mmoja kwenye kichwa cha mtoto ili kukilegeza. Tumia mkono wako mwingine kushikilia periniamu. Mfunze wanawake mbinu za kupumua ili kusukuma au kukoma kusukuma.

11.4.1 Hatua za dharura katika utunzaji wa waakati wa ujauzito

11.4.3 Hatua za dharura katika na baada ya awamu ya tatu ya leba