11.5 Udhibiti wa dharura wa kuvuja damu baada ya kuzaa

Iwapo mama ataanza kuvuja damu kupita kiasi baada ya kuzaa, chukua hatua ya haraka na umsafirishe hadi katika kituo chochote cha afya kilicho karibu. Kuvuja damu baada ya kuzaa kunaweza kusababisha kifo. Wahudumu wengi wa afya hupuuza kiwango cha damu anachopoteza mwanamke. Ukikumbana na tatizo hili, kwanza paza sauti ukiomba usaidizi. Paza sauti uwaite familia au majirani wakusaidie kumpeleka katika kituo kilicho karibu cha afya (Mchoro 11.4).

Mchoro 11.4 Usikawie kumpa rufaa mwanamke aliyevuja damu nyingi baada ya kuzaa.

11.4.3 Hatua za dharura katika na baada ya awamu ya tatu ya leba

11.5.1 Dawa za kukazisha uterasi na viowevu vya mishipa ya vena katika kudhibiti kuvuja damu kwa baada ya kuzaa kunakohusiana na mikazo