11.5.2 Tumia mbinu ya shinikizo la mikono miwili kwenye uterasi

Ikiwa damu inatoka kwa wingi na kusugua hakusimamishi kuvuja huku kwa damu, jaribu shinikizo la mikono miwili kwenye uterasi (Mchoro 11.5). Chota uterasi, ikunje upande wa mbele kisha uifinye kwa nguvu. (Ulionyeshwa jinsi ya kufanya hivyo katika masomo ya ustadi ya utendaji). Shikilia mkono mmoja juu ya uterasi. Weka mkono wako mwingine kwenye mfupa wa kinena na uisukume uterasi mbele kuelekea katika mkono wa kwanza. Ifinye uterasi katikati ya mikono yako.

Ikiwa umefunzwa kufanya hivi, unaweza kuifinya uterasi kwa mikono miwili kwa kufuata mbinu hii. Ingiza mkono wako mmoja ulio na glavu kwenye uke kisha ukaze mkono wako nyuma ya seviksi. Finyilia huo mkono mwingine kwenye fumbatio ili kuibana uterasi.

Mchoro 11.5 Shinikizo la mikono miwili juu ya uterasi linaweza kukomesha kuvuja damu baada ya kuzaa.

Punde tu damu itakapopungua kuvuja na unahisi kuwa uterasi iko dhabiti, sitisha shinikizo hili la mikono miwili taratibu. Ikiwa damu itaendelea kuvuja, mpe rufaa mwanamke huyu hadi katika kituo kilicho karibu cha afya. Jaribu kutumia shinikizo la mikono miwili juu ya uterasi wakati unamsafirisha mama huyu. Usimwache mtoto nyumbani. Hakikisha kuwa mtu mwingine amembeba mtoto. Hakikisha umeandamana na watu wanaoweza kumtolea mwanamke damu kutoka kwa jamaa yake. Mwanamke huyu anaweza kuhitaji kuongezwa damu.

11.5.1 Dawa za kukazisha uterasi na viowevu vya mishipa ya vena katika kudhibiti kuvuja damu kwa baada ya kuzaa kunakohusiana na mikazo

11.5.3 Udhibiti wa dharura wa kuvuja damu baada ya kuzaa kunakohusiana na jeraha