11.5.3 Udhibiti wa dharura wa kuvuja damu baada ya kuzaa kunakohusiana na jeraha

Mwanamke huyu anaweza kuwa na jeraha, kama vile mchibuko kwenye periniamu au uke. Ili kusitisha kuvuja kwa damu kutoka kwenye jeraha, weka shinikizo juu ya sehemu inapovujia damu. Kunja vipande 10 hadi 15 vya shashi iliyotakaswa au kitambaa kidogo kilichotakaswa katika pedi nene. Ifinyilie pedi hii kwa nguvu kwenye sehemu ya mchibuko inayovuja damu. Ishikilie pedi humo kwa dakika 10. Kwa umakinifu, iondoe shashi hii kisha udhibitishe kama damu ingali inavuja. Ikiwa mchibuko bado unavuja damu, ifinyilie shashi hii tena kwenye sehemu inayovujia kisha umpeleke mwanamke huyu katika kituo kilicho karibu cha afya. Endelea kuweka shinikizo juu ya mchibuko huu hadi utakapofika katika kituo cha afya. Ikiwa mwanamke huyu ana mchibuko mrefu au ulioingia dani sana, mpeleke katika kituo cha afya ambapo mchibuko huu unaweza kurekebishwa. Mpeleke hata ikiwa damu inavuja kwa kiwango cha chini kutoka kwenye mchibuko huu.

11.5.2 Tumia mbinu ya shinikizo la mikono miwili kwenye uterasi

11.6 Orodha ya ithibati za rufaa ya dharura