Muhtasari wa Kipindi cha 11

Katika Kipindi cha 11, umesoma yafuatayo:

  1. Hali ya kuvuja damu baada ya kuzaa ni mojawapo ya visababishi vikuu vya vifo vinavyotokana na kuzaa katika nchi zinazostawi. Ni vigumu kutabiri ni wanawake wepi watakaokumbwa na hali hii, kwa hivyo unafaa kuwa tayari kuidhibiti kila unapozalisha.
  2. Visa vingi vya hali hii vinaweza kuzuiliwa kupitia utunzaji wa kiustadi wakati wa ujauzito, leba na kipindi kinachofuatia kuzaa.
  3. Wakati wa utunzaji wa kabla ya kuzaa, wanawake wote wajawazito wanafaa kupokea ushauri kuhusu lishe na kinga dhidi ya malaria. Wanawake wote wajawazito wanafaa kupokea matibabu dhidi ya mnyoo. Wanawake hawa pia wanafaa kupokea nyongeza ya virutubishi vya madini ya chuma/foleti ili kuzuia anemia, ambayo ni kipengele hatari cha kuvuja damu baada ya kuzaa.
  4. Mpe rufaa mapema ikiwa leba itakawia. Dhibiti jinsi kichwa kinavyotoka wakati wa kuzaa katika awamu ya pili ili kuzuia kuvuja damu baada ya kuzaa kunakohusiana na majeraha.
  5. Baada ya mtoto kuzaliwa, mpe mama misoprostol au oxytocin ili kuzuia kuvuja damu baada ya kuzaa kunakohusiana na mikazo, kisha upapase uterasi baada ya plasenta kutoka.
  6. Kuvuja damu baada ya kuzaa kukiendelea, tambua kisababishi cha kuvuja huku. Ikiwa kuvuja damu baada ya kuzaa kumesababishwa na uterasi isiyojikaza (iwe plasenta imesalia au la), ipapase uterasi ukitumia mikono miwili. Ondoa mkojo kutoka kibofuni (ikiwa inahitajika, tumia katheta) na uandae kiowevu cha vena. Mpe ama kipimo cha pili cha oxytocin 10 IU kwa kumdunga ndani ya misuli au kipimo cha pili cha misoprostol miligramu 400 kupitia rektamu au uzitie tembe hizi chini ya ulimi wake.
  7. Ikiwa hali hii inasababishwa na majeraha, tumia shinikizo dhabiti kwa dakika kumi kwenye sehemu inayovujia damu ukitumia pedi safi. Ikiwa damu itaendelea kuvuja, anzisha tena shinikizo na umpe rufaa hadi katika kituo cha afya ambapo jeraha hili linaweza kutibiwa.
  8. Kaa na mwanamke huyu katika kituo cha afya ambapo umempeleka rufaa. Chunguza dalili muhimu, dumisha shinikizo la uterasi na umpe joto na usaidizi wa kihisia.

11.6 Orodha ya ithibati za rufaa ya dharura

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 11