Malengo ya Kipindi cha 1

Baada ya kipindi hiki unafaa uweze;

1.1 Kufafanua na kutumia kwa usahihi maneno yote yaliyoandikwa kwa hefufi nzito (maswali ya kujitathmini 1.1, 1.2 na 1.4)

1.2 Kulinganisha kiwango cha vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na vya watoto wachanga na matatizo barani Afrika na hali ilivyo ulimwenguni kote na Afrika kwa jumla (maswali ya kujitathmini 1.1)

1.3 Kujua jinsi ya kukadiria idadi ya wanawake wajawazito watakaohitaji utunzaji katika ujauzito katika jamii yako kwa mwaka mmoja (maswali ya kujitathmini 1.2)

1.4 Kujua jinsi ya kupanga mpango wa utunzaji katika ujauzito ulionuiwa wa mara nne kwa kila mwanamke mjamzito kwa muda maalum katika eneo lako (maswali ya kujitathmini 1.3)

1.5 Kujua jinsi ya kukokotoa kiwango cha matumizi ya huduma za utunzaji katika ujauzito na sehemu ya waliozaa kwa kuhudumiwa na mtaalamu wa afya katika eneo lako (maswali ya kujitathmini 1.2)

1.6 Kujua jinsi ya kukokotoa uwiano wa vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na wa vifo vya watoto wachanga katika eneo lako (maswali ya kujitathmini 1.4)

Kipindi cha 1 Kupanga Utunzaji katika Ujauzito

1.1 Vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na vya watoto wachanga