21. Kuvuja Damu katika Awamu za Mwisho wa Ujauzito

Kipindi cha 21 Kuvuja Damu katika Awamu za Mwisho wa Ujauzito

Utangulizi

Kuvuja damu baada ya wiki 28 za ujauzito hukisiwa kuwa kuvuja damu katika awamu za mwisho wa ujauzito. Ulijifunza kuhusu kuvuja damu katika awamu za mwanzo kabla ya wiki 28 za ujauzito katika Kipindi cha 20. Kuvuja damu katika awamu za mwisho za ujauzito pia hujulikana na madaktari na wakunga kama kuvuja damu kabla ya kuzaa. Hali hii ni kisababishi kikuu cha vifo vya kina mama na fetasi, hivyo huhitaji usaidizi wa mtaalamu wa huduma ya afya haraka iwezekanavyo ili kuokoa maisha ya mwanamke na mtoto wake ambaye bado hajazaliwa.

Wewe kama mhudumu wa afya wa kwanza kufikiwa na wanawake wajawazito katika jamii yako, unapaswa kushirikiana nao katika maandalizi ya kuzaa na kufanya mpango unaoshugulikia matatizo yoyote katika ujauzito, kama vile kuvuja damu kwa wingi. Unapaswa kutoa huduma ya kwanza ya kiukunga kisha uhakikishe kuwa mwanamke anayevuja damu katika awamu za mwisho wa ujauzito amefikishwa kituoni cha afya ili apate huduma ya dharura. Hospitali ya Wilaya au Kituo cha Afya chenye uwezo wa kufanya upasuaji wa kiukunga kinaweza kuokoa maisha yake.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 21