2. Kuendeleza Utunzaji katika Ujauzito

Kipindi cha 2 Kuendeleza Utunzaji katika Ujauito

Utangulizi

Katika somo hili utajifunza tofauti kati ya kuendeleza afya, elimu ya kiafya,uchunguzi wa kiafya na kuzuia magonjwa. Pia utajifunza njia tofauti za kuwasilisha jumbe za elimu ya kiafya kwa heshima na huruma.

Pia utajifunza jinsi ya kuelimisha na kushirikisha watu binafsi, vikundi, viongozi mashuhuri na wanajamii katika uendelezaji na utumiaji bora wa huduma za utunzaji katika ujauzito. Kanuni zizi hizi zinaweza pia kutumika katika kuendeleza utumiaji wahuduma za afya wakati wa uchungu wa kuzaa, katika kuzaa na baada ya kuzaa - utakavyoona katika moduli mbili zifuatazo. Hatimayetutakuonyesha hatua katika kupanga shughuli za elimu ya kiafya zinazolenga kupunguza vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na vya watoto wazawa kwa kuongeza kiwango cha utunzaji katika ujauzito. Unaweza kutumia hatua zizi hizi kwa shughuli za kuendeleza afya ukiwa na malengo mengine, kwa mfano, ya kuongeza kiwango cha utumiaji wa huduma za kupanga uzazi.

Malengo ya Somo laKipindi cha 2