7. Mabadiliko ya Kifiziolojia katika Ujauzito

Kipindi cha 7 Mabadiliko ya Kifiziolojia katika Ujauzito

Utangulizi

Wakati wa ujauzito, mwili wa mwanamke hubadilika kwa njia mbalimbali kufuatia athari za homoni. Wakati mwingine mabadiliko haya huwa sumbufu, lakini mara nyingi ni mabadiliko ya kawaida ambayo humwezesha mwanamke kulisha na kulinda fetasi, kuandalia mwili wake na kuandalia matiti yake ili yaweze kutoa maziwa.

  • Je, unakumbuka fasili ya homoni katika Kipindi cha 3?

  • Homoni ni kemikali ashirizi zinazozalishwa mwilini, ambazo husafirishwa katika damu. Homoni mbalimbali hudhibiti au kurekebisha utendakazi wa seli au viungo tofauti.

    Mwisho wa jibu

Katika Kipindi hiki, utajifunza kuhusu baadhi ya mabadiliko yanayotokea wakati wa ujauzito katika uterasi, seviksi na uke, mfumo wa moyo na mishipa ya damu, mfumo wa tumbo na utumbo mdogo na mfumo wa mkojo, na pia kuhusu mabadiliko kwenye matiti na ngozi. Pia utajifunza kuhusu madhara ya mabadiliko haya yote kama utavyohitaji kufahamu kama mhudumu wa afya anayeshughulikia afya ya wajawazito. Kwa kuelewa mabadiliko ya kawaida ya ujauzito, unaweza kumhakikishia mwanamke ikiwa ana wasi wasi, na pia kumchunguza na kumhudumia kwa haraka zaidi ikiwa utagundua chochote kisicho kawaida. Elimu ya kimsingi ya mabadiliko na virekebishi hivi pia ni muhimu katika kuelewa Malengo ya uchunguzi wa kimaabara unaoweza kufanywa katika kituo cha afya katika kipindi cha ujauzito.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 7