8. Kutambua Ujauzito na Kujifunza Historia ya Mwanamke Mjamzito

Kipindi cha 8 Kutambua ujauzito na Kujifunza Historia ya Mwanamke Mjamzito

Utangulizi

Kipindi hiki kinaanza kwa kukupa maarifa ya kutambua mwanamke awapo mjazito. Utajifunza kutofautisha kati ya ishara na dalili zinazoweza kuashiria ujauzito, zinazoelekea kuashiria ujauzito na zile chanya. Dalili ni kiashiria cha hali fulani (kama vile ujauzito), au ugonjwa au tatizo kinachogunduliwa na mhusika, na anachoweza kuelezea mwenyewe, au ukiuliza maswali mwafaka. Kwa upande mwingine, ishara ni kiashiria kinachoweza kugunduliwa na mtaalam wa maswala ya afya tu, au kwa kupima.

Ili kumpa mwanamke mjamzito utunzaji bora, unahitaji pia kujua kuhusu hali yake ya kiafya kwa jumla na ujauzito wa hapo awali na ni mara ngapi ameweza kuzaa na hali ya ujauzito huu kufika sasa. Habari hizi huitwa historia ya kitiba. Mchakato wa kukusanya habari yote na kuinakili kwa kutumia maswali wazi na yanayoeleweka huitwakuchukua historia. Katika Kipindi hiki utajifunza jinsi ya kuuliza maswali barabara kuhusu historia ya kiafya ya mwanamke mjamzito. Maarifa haya yatakusaidia kutoa ushauri mwafaka na wa kibinafsi ili kuuwezesha ujauzito na uzazi huu kuwa salama iwezekanavyo. Pia utatambua umuhimu wa kudumisha imani ya mwanamke kwa kuweka anayokuambia kwa siri.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 8