18. Matatizo ya Kiafya ya Kawaida wakati wa Ujauzito

Kipindi cha 18 Matatizo ya Kiafya ya Kawaida wakati wa Ujauzito

Utangulizi

Katika kipindi hiki, utajifunza kuhusu matatizo matatu ya kawaida ya kiafya wakati wa ujauzito na athari zake kwa afya ya mjamzito: malaria, anemia na maambukizi kwenye njia ya mkojo na jinsi ya kutofautisha maambukizi ya njia ya mkojo (MNM) yanayoweza kutibiwa kutokana na yale yanayoendelea kwa kibofu cha mkojo na ugonjwa kali unoathiri figo. Tutakueleza visababishi, ishara, dalili, utambuzi, na udhibiti wa hali hizi, na wakati wa kumpa mama rufaa kwa kituo cha afya kwa uchunguzi na matibabu zaidi. Na utajifunza njia bora za kuzuia hali hizi zisitokee na umuhimu wa kufanya hivyo hasa wakati wa ujauzito.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 18