3. Anatomia na Fiziolojia ya Mfumo wa Uzazi wa Kike

Kipindi cha 3 Anatomia na Fiziolojia ya mfumo wa Uzazi wa Kike

Utangulizi

Anatomia na fiziolojia kwa huduma ya kimsingi ya ukunga ni utangulizi katika masomo yako kwenye Moduli hii na nne zifuatazo, na pia ni maandalizi muhimu kwa mafunzo yako. Huduma ya ukunga ni utunzaji wa kiafya kwa wanawake katika ujauzito, leba, kuzaa na huduma ya baada ya kuzaa. Huduma hii huhitaji ufahamu mwafaka wa anatomia na fiziolojia ya mfumo wa uzazi wa kike. Anatomia ni taaluma ya viungo vya mwili wa binadamu, yaani, jinsi viungo, tishu na mifumo ya mwili inavyoundwa. Fiziolojia kwa upande mwingine, ni taaluma inayohusu jinsi viungo, tishu, na mifumo ya viumbehai inavyofanya kazi mwilini.

Katika Kipindi hiki, utajifunza kuhusu viungo vinavyounda Sehemu ya siri za nje za kike na viungo vya ndani vya uzazi. Katika Kipindi cha 4, tunakufunza kuhusu jinsi homoni zinavyoratibisha viungo vya ndani vya uzazi wa kike na mzunguko wa hedhi. Katika Kipindi cha 5, tunaeleza ovulesheni, utungisho, pandikizo la kiinitete kwenye uterasi ya mama, ukuaji wa fetasi, planseta na lishe ya fetasi. Katika Kipindi cha 6, utajifunza anatomia ya pelvisi ya kike na pia ya fuvu la fetasi, ambayo sharti ipitie kwenye pelvisi ya mama wakati wa kuzaa.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 3