6. Maumbile ya Pelvisi ya Mwanamke na Fuvu la Fetasi

Kipindi cha 6 Maumbile ya Pelvisi ya Mwanamke na Fuvu la Fetasi

Utangulizi

Katika Kipindi hiki, utajifunza kuhusu miundo ya kimifupa iliyo mihumu zaidi katika mwanamke mjamzito na mtoto atakayemzaa. Kazi kuu ya mifupa ya kiunzi ni kuegemeza uzito wa mwili na kutenda kazi kama sehemu za kuunganisha misuli. Lengo la somo hili ni kuhusu pelvisi ya mwanamke, ambayo huegemeza sehemu kubwa ya uzito wa uterasi inayobeba mimba, na fuvu la fetasi, ambalo ni sharti lipitie katika pelvisi ya mwanamke anapozaa.

Kuna sehemu kuu mahususi katika maumbile ya pelvisi ya mwanamke na fuvu la fetasi ambazo tutakuonyesha katika Kipindi hiki. Kufahamu sehemu hizi kuu kutakuwezesha kukadiria jinsi leba inavyoendelea, kwa kutambua mabadiliko katika hali zake linganifu huku mtoto akishukia katika njia ya uzazi. (Utajifunza kuhusu haya yote katika Moduli inayofuata ya Leba na Utunzaji wakati wa Kuzaa.)

Malengo ya Somo la Kipindi cha 6