1.1 Vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na vya watoto wachanga

Tunaanza kipindi hiki kwa kueleza idadi ya kina mama na watoto wachanga wanaofariki kutokana na matatizo ya ujauzito na kuzaa duniani. Shirika la Afya Duniani liliweka malengo ya milenia ya maendeleo mwaka wa 2000 (1992 katika kalenda ya Afrika) ili kupunguza kwa robo tatu vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa katika kila nchi na kwa theluthi mbili vifo vya watoto walio chini ya miaka 5 kufikia mwaka 2015 (2007 katika kalenda ya Afrika). Afrika ni mojawapo ya bara chache duniani inayotarajiwa kutimiza malengo haya kwa kupunguza vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na vya watoto. Jukumu lako kama mtalamu wa afya ni muhimu katika kutimiza malengo haya.

Tarehe zote zilizo katika moduli hii zinatumia mfumo wa kalenda ya Uropa na Amerika.

Malengo ya Kipindi cha 1

1.1.1 Vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na matatizo