1.1.3 Je, vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na vya watoto wachanga vinawezaje kupunguzwa?

Kupunguza vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na vya watoto wachanga vimetambuliwa kimataifa kama mojawapo ya malengo ya milenia ya maendeleo yaliowekwa mwaka wa 2000 na shirika la afya duniani. Inakadiriwa kuwa tunaweza kuzuia karibu asilimia 75 ya vifo vya watoto wachanga, zaidi ya asilimia 50 ya vifo katika mwaka wa kwanza wa maisha, na asilimia 99 ya vifo vya kina mama katika ujauzito kwa kuboresha afya na lishe ya mama mjamzito kupitia utunzaji katika huduma ya baada ya kuzaa moja kwa moja. Maendeleo haya yanaweza kutimizwa kupitia utatuzi unaofaa wa kijamii, ambao ni mawasiliano yanayofaa na elimu ya afya juu ya utunzaji kabla ya kuzaa (imeangaziwa katika kipindi cha 2). Kutambua na kudhibiti kwa mapema wa matatizo ya kiafya wakati wa ujauzito (kumeangaziwa katika vipindi vya baadaye katika moduli hii), na kuhusu huduma wakati wa uchungu wa kuzaa, wakati wa kuzaa, kipindi cha baada ya kuzaa, na kudhibiti maradhi ya watoto wachanga na yale ya utotoni (katika moduli tatu zifuatazo).

1.1.2 Vifo vya watoto wachanga na matatizo

1.2 Kupangia mama mjamzito na mtoto mchanga utunzaji wa kiafya katika jamii yako