1.2.4 Kukokotoa kiwango cha utumiaji wa huduma zifaazo katika ujauzito

Kiwango cha waliopata huduma zifaazo katika ujauzito ni sehemu ya idadi ya wanawake wajawazito waliohudumiwa angalau mara moja katika ujauzito wa wakati huo na mtaalamu wa afya kama vile mhudumu wa afya wa nje ya hospitali, kwa mujibu wa sababu zinazohusiana na ujauzito huo. Kukokotoa awamu za kwanza za huduma zifaazo kwa kina mama wajawazito hutoa habari juu ya asilimia ya wanawake wanaozitumia huduma zifaazo katika ujauzito.

Kiwango cha waliopata huduma zifaazo katika ujauzito hukokotolewa kama idadi kamili ya wanawake wajawazito waliohudumiwa angalau mara moja na mtaalamu wa afya kwa mujibu wa sababu zinazohusiana na ujauzito huo zikigawanywa na idadi kamili ya ujauzito unaotarajiwa kwa kipindi fulani cha muda (Kwa kawaida mwaka mmoja) katika eneo hilo. Jibu huwasilishwa kama asilimia kwa kuzidisha na 100.

Kwa mfano, ikiwa idadi kamili ya awamu za kwanza za kabla ya kuzaa ni 100, na idadi kamili ya ujauzito ni 200, basi kiwango cha waliopata huduma zifaazo katika ujauzito katika jamii yako itakuwa asilimia 50, kokotoa jinsi ilivyoandikwa hapa chini:

  • Je, ni kwa nini unafikiri ukokotozi wa kiwango cha huduma zifaazo katika ujauzito katika jamii yako ni muhimu?

  • Inakuwezesha wewe pamoja na msimamizi wako kuona ikiwa juhudi zenu za kuendeleza matumizi ya huduma zifaazo katika ujauzito zina mafanikio. Kwa mfano, kama kiwango cha huduma hizi ni asilimia 50 ya wanawake wajawazito kabla kuanza kampeni ya kuendeleza afya ili kuongeza matumizi ya huduma hizi, mnaweza kudai kuwa kampeni yenu ilikuwa na mafanikio ikiwa matumizi ya huduma hizi yaliongezeka kufikia asilimia 60 au zaidi.

    Mwisho wa jibu

1.2.3 Kukokotoa idadi ya vipimo vilivyonuiwa vya utunzaji katika ujauzito

1.2.5 Kukokotoa sehemu ya wanawake waliozaa kwa kuhudumiwa na` wataalamu wa afya