1.2.6 Kukokotoa uwiano wa vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa

Uwiano wa vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa hufafanuliwa kama idadi ya vifo vya kina mama hawa kakatika mwaka na eneo fulani (hii inaweza kuwa nchi nzima, eneo au jamii kama vile jamii yako), ikigawanywa na idadi ya watoto waliozaliwa wakiwa hai katika mwaka huo na eneo hilo. Jibu huzidishwa mara 100,000 ya watoto wanaozaliwa wakiwa hai ili iweze kulinganishwa na miaka mingine na maeneo mengine.

  • Katika eneo X mwaka wa 2002 kulikuwa na vifo 10 vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa na vifo vya watoto waliozaliwa wakiwa hai 10,000. Je kiwango cha vifo (katika asilimia) vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa katika eneo X kwa kila watoto 10,000 waliozaliwa wakiwa hai mwaka huo ni nini?

  • Mwisho wa jibu

  • Je, uwiano huu wa vifo vya kina mama kabla , katika na muda mfupi baada ya kuzaa unalinganaje na uwiano wa vifo hivi katika bara la Afrika mwaka wa 2005?

  • Ni mdogo mno ukilinganishwa na uwiano wa vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa wa Afrika ambao ni 673 kwa kila watoto 100,000 wanaozaliwa wakiwa hai kwa mwaka huo. Kama asilimia hii ingekuwa imetimizwa katika nchi nzima ya Afrika, Malengo ya Milenia ya maendeleo ya kupunguza vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa kwa robo tatu kufikia mwaka wa 2015 yangekuwa yametimizwa kwa kiwango kikubwa.

    Mwisho wa jibu

1.2.5 Kukokotoa sehemu ya wanawake waliozaa kwa kuhudumiwa na` wataalamu wa afya

1.2.7. Kukokotoa kiwango cha vifo vya watoto wachanga