2.1 Uendelezaji wa afya

Uendelezaji wa afya ni shughuli zozote zinazosababisha afya bora katika jamii au nchi. Huhusisha jinsi ya kuwawezesha watu kuongeza udhibiti na uboreshaji wa afya yao. Lakini huenda zaidi ya kuzingatia mienendo ya mtu binafsi kuelekea utatuzi anuwai wa kijamii na kimazingira ambao huboresha afya. Uendelezaji wa afya huhusisha vitendo vyovyote vya watu binafsi, mashirika ya kijamii, ofisi za afya katika wilaya na maeneo, na serikali yanayolenga kuboresha afya ya watu wao. Kwa mfano, ujenzi wa hospitali zaidi na vituo vya afya, kufunza wahudumu wa afya zaidi ni shughuli za kuendeleza afya kitaifa. Vile vile ilivyokuhakikisha kuwa kila mmoja katika nchi anapata chakula cha kutosha, nyumba na maji safi.

Uendelezaji wa afya katika jamii huhusisha shughuli za aina tatu(jedwali 2.1). Tutaanza kwa kuangazia mifano ya kila moja ya aina hizi kwa zamu.

Jedwali 2.1 kuendeleza afya katika jamii kunahusisha elimu ya kiafya, uchunguzi wa kiafya na shughuli za kuzuia magonjwa.

Elimu ya kiafya ni uwasilishaji wa habari sahihi na muhimu za afya kwa wanajamii. Huwawezesha watu binafsi na vikundi kukuza maarifa yao ya masuala ya afya, kuongeza kujitegemea na uwezo wao wa kusuluhisha matizo yao ya kiafya kupitia ari yao yenyewe. Kibainishi kikuu cha afya bora au duni ni elimu ambayo watu wanayo kuhusu masuala ya afya, imani zao, mitazamo, mienendo yao na nia ya kusababisha mabadiliko ya kimienendo katika maisha yao.

Jukumu muhimu kwako kama muhudumu wa afya ni kutoa elimu mwafaka ya kiafya kwa watu katika jamii yako ili waweze kujadiliana nawe na miongoni mwao matatizo yao ya kiafya kisha wafanye uamuzi ufaao ili kuboresha afya yao na ya jamaa zao kwa juhudi zao wenyewe. Kwa hivyo elimu ya kiafya ni zana muhimu kwa kuwaleta watu katika utendaji. Ikiwa elimu ya kiafya itawasilishwa katika mpango uliopangwa na kuratibiwa vizuri na kuungwa mkono na kushiriki kwa jamii hakutakuwa na njia bora ya kuhimiza mienendo bora ya kiafya na kutatua au kuzuia matatizo mengi ya afya yanayotokea mara kwa mara.

  • Je, mienendo ni nini na hutokea wapi?

  • Mienendo ni kile watu wanatenda au kuzoea katika maisha yao ya kila siku. Chanzo chake ni maisha yetu ya kila siku, mazingira yetu na matukio tuliyolimbikiza na kufahamishwa na imani, tamaduni, mila na tabia zetu.

    Mwisho wa jibu

Mienendo ifaayo ya kiafya ni tendo lolote la mtu binafsi linaloboresha afya yake au afya ya wengine katika jamii.

  • Je, unaweza kupendekeza baadhi ya mifano ya mienendo ifaayo ya kiafya?

  • Unaweza kuwa umefikiria mifano kama vile kula lishe bora, kufanya mazoezi ya kutosha, kulala usingizi wa kutosha usiku na kujiepusha na mienendo inayoharibu afya kama vile kuvuta tumbaku, kunywa pombe kwa wingi au kushiriki ngono bila kondomu.

    Mwisho wa jibu

Sanduku la pili katika jedwali 2.1 linaonyesha uchunguzi wa kiafya ambao ni utaratibu wa kupimwa kwa watu binafsi ili kujua ikiwa wako katika hatari ya kukumbwa na tatizo la kiafya. Uchunguzi wa kiafya ni shughuli muhimu ya kuendeleza afya utakayofanya kama mojawapo ya huduma za utunzaji katika ujauzito. Kwa mfano, utapima halijoto, shinikizo la damu na mdundo wa moyo wa kila mwanamke mjamzito kila anapotembelea huduma hizi (tutakuonyesha jinsi ya kufanya haya katika Kipindi cha 9 cha somo) ili kujua ikiwa ana tatizo la kiafya linaloweza kumdhuru yeye au mtoto wake.

Sanduku la mwisho katika jedwali 2.1 linaonyesha uzuiaji wa magonjwa. Hii hurejelea tendo lolote linalofanywa kwa minajili ya kuzuia kukua kwa ugonjwa. kwa mfano, kumpa mwanamke mjamzito madini ya ziada kama mojawapo ya utaratibu wa utunzaji katika ujauzito ni tendo la kuzuia ukuaji wa anemia. Anemia ni hali inayoufanya mwili kutengeneza seli nyekundu za damu chache mno kwa sababu lishe ya mwanamke huyo haina madini ya kutosha. (Utajifunza jinsi ya kugundua na kutibu anemia katika vikao vya 9 na 18 vya somo katika moduli hii.)

Unaweza kuona katika majadiliano hapo juu ya kwamba kuendeleza afya huhusisha shughuli anuwai. Katika masomo yatakayofuata katika moduli hii, utajifunza mengi kuhusu elimu maluum ya kiafya, uchunguzi wa kiafya na shughuli za kuzuia magonjwa ambazo huchangia katika utunzaji katika ujauzito kwa wanawake wajawazito katika jamii yako. Katika Kipindi hiki cha somo tutaangazia kanuni za jumla za elimu ya kiafya kama kipengele muhimu cha kuendeleza afya katika utunzaji katika ujauzito.

Malengo ya Somo laKipindi cha 2

2.2 Kuelimisha jamii yako kuhusu utunzaji katika ujauzito