2.3 Mbinu za kuwasilisha jumbe za afya

2.3.1  Mbinu ya kutoa na kupokea habari

Ili kuendeleza matumizi bora ya huduma za utunzaji katika ujauzito, mawasiliano yafaayo hutekeleza wajibu muhimu. Mbinu za mawasiliano ni njia zote ambazo watu hutumia kwa kubadilishana mawazo, hisia na habari kupitia mazungumzo, chapa kama vile vitabu na kurasa zenye matangazo, mabango, redio, runinga na kwa kiwango kikubwa kupitia mtandao kukiweko vifaa. Elimu ifaayo ya kiafya huhusisha mazungumzo ya kutoa na kupokea habari.

  • Je, mawasiliano ya kutoa na kupokea habari ni nini?

  • Hutendeka wakati habari inabadilishwa kati ya angalau watu wawili kupitia kushiriki na majadiliano.

    Mwisho wa jibu

Mawasiliano ya kutoa na kupokea habari ni njia bora ya kuendeleza jumbe za elimu ya kiafya kwa watu binafsi au vikundi. Sharti kuwe na mtiririko huru wa mawasiliano kati ya wahusika wote. Kumbuka kwamba masikio yako ni baadhi ya zana zako muhimu. Hii ni muhimu hasa katika elimu ya afya kwa sababu inakuwezesha kupata majibu muhimu ya utekelezaji wa maazimio kutoka kwa kila mtu, kuelewa matatizo yao na kuyatatua kupitia majadiliano.

  • Je, ni wapi na lini elimu juu ya afya ya wanawake wajawazito hutolewa?

  • Inaweza kutolewa pahali popote na wakati wowote. Kwa mfano, wakati wa kupimwa katika utunzaji katika ujauzito, ukiwa unauliza maswali na kusikiliza majibu ya mwanamke, unaweza kujadili masuala ambayo ni muhimu kwake. Sokoni, katika mkutano wa jamii (Picha 2.2) au kila unapokutana na wanawake wajawazito au waume zao.

    Mwisho wa jibu

Picha 2.2 Mikusanyiko mbalimbali ya jamii ni nyakati nzuri za kupitisha jumbe za kiafya.

Wahusishe wanaume na wanawake katika kujadili faida za utunzaji katika ujauzito.

2.2 Kuelimisha jamii yako kuhusu utunzaji katika ujauzito

2.3.2 Chagua mbinu za mawasiliano zitakazoifaa hadhira yako