2.3.3 Utetezi na uhamasishaji wa jamii

Utetezi ni kutetea au kutenda kwa niaba yako mwenyewe au mtu mwingine. Uhamasishaji wa jamii unarejelea mfumo mpana wa muungano wa kuwahusisha watu kushiriki katika kutimiza lengo maalum kupitia bidii za kibinafsi. Utetezi na uhamasishaji wa jamii utakusaidia kupata na kuendeleza ushirikishaji wa watu wenye ushawishi mkubwa, vikundi na sekta katika nyanja tofauti katika jamii watakaounga mkono mipango ya utunzaji katika ujauzito.

Mikakati hii imeangaziwa kwa kina katika moduli juu ya Elimu ya Afya, Utetezi na Uhamasishaji wa jamii.

Ukifanikiwa katika kuwafundisha watetezi kuongea kwa uwazi kuhusu utunzaji katika ujauzito na uhamasishaji wa uungwaji mkono pakubwa wa huduma hii, matokeo yanaweza kuwa;

  • Kuboresha uwezekano wa wanawake wajawazito kufikia huduma zifaazo katika ujauzito na kukubalika kwa huduma hizi katika jamii
  • Kuandaa mabaraza ya kujadili na kuratibu huduma zifaazo katika ujauzito
  • Uhamasishaji juu ya rasilimali za jamii kama vile usafirishaji, utoaji wa habari na fedha za dharura kwa wanawake wajawazito na wanaopata matatizo katika uchungu wa kuzaa yanayohitaji huduma ya kiafya kwa dharura.

Viongozi mashuhuri kama watetezi wa utunzaji katika ujauzito.

Kuhusisha usaidizi wa watetezi ambao ni viongozi mashuhuri au watu muhimu katika eneo lako ni jukumu muhimu. Wazee wanaojulikana na wenye kuheshima, viongozi wa kitamaduni au wa dini na watu wenye hekima ambao ushauri na maneno yao yana kibali katika jamii na wanaweza kuwashawishi wengine kuhusu faida za utunzaji katika ujauzito kwa kushinikiza jamii. Mazoea ya wanajamii kukubaliana nao ni muhimu kwa kuwasilisha jumbe za kiafya na kupata kibali kutoka kwa wengine.

Unaweza kutumia viongozi hawa walio heshimika kuwasilisha jumbe zifaazo kuhusu utunzaji katika ujauzito ikiwa utawapa habari ifaayo na uko tayari kuwatumia kama watetezi. Utetezi kutoka kwa viongozi walio heshimiwa unaweza kukuhakikishia kuwa watu wanazingatia na kuendeleza mienendo ifaayo uliyoleta kupitia elimu ya kiafya.

Jaribu kupata idadi ya juu zaidi ya watu wanaohusika katika uenezaji wa huduma za utunzaji katika ujauzito ili jamii iweze kuimarisha uungaji mkono wa afya ya wanawake wajawazito (Picha 2.3)

Picha 2.3 Uhamasishaji wa jamii kuunga mkono utunzaji katika ujauzito huhusisha jamii nzima, kwa sababu afya ya mwanamke mjamzito inaweza kukingwa au dhuriwa na yeyote.

Wanaume kama watetezi wa utunzajii ufaao katika ujauzito

  • Je, wanaume wana wajibu katika utunzaji katika ujauzito?

  • Ndio! Kuhusika kwao ni muhimu kwa sababu wanaume wanaweza kushawishi ikiwa wanawake wajawazito katika familia zao wanatembelea huduma za utunzaji katika ujauzito ili kupimwa mara kwa mara na kufuata ushauri wako.

    Mwisho wa jibu

Wahimize wanaume iwezekanavyo kushiriki katika kuboresha afya ya wanawake. Waume, kina baba, watoto wa kiume, viongozi wa jamii, viongozi wa kidini, mabosi na wanaume wengine wote huchangia jinsi afya ya wanawake itakavyokuwa kwa mujibu wa ujauzito, uchungu wakati wa kuzaa na katika kuzaa. Jamii nzima itafaidika ikiwa wanaume katika jamii watahisi kuwajibikia afya ya wanawake. Kwa hivyo wasaidie wanaume kuhusishwa katika kuendeleza utunzaji katika ujauzito.

Endeleza majukumu na ujuzi ambao wanaume tayari wanao. kwa mfano, katika jamii nyingi, wanaume hutazamiwa kama walinzi. Wasaidie wanaume wajifunze jinsi ya kulinda afya ya wanawake. Wahimize wanaume kushiriki katika majukumu ya ujauzito na malezi. Wanaume wanaweza kuwatunza watoto sawa na wanawake kwa kuliwaza, kuogesha, kuwapa chakula, kuwafunza na kucheza nao. Waalike wanawake na wanaume katika mikutano ya kijamii na uwahimize wanawake waongee. Wakati mwingine wanawake husita kuongea kuhusu ujauzito na mambo ya kuzaa mbele ya wanaume.

Shirikiana na wanaume walio na huruma kwa mahitaji ya wanawake. Wanaume hawa wanaweza kusemezana na wanaume wengine ambao huenda wamsikize mwanamume kwa makini kuliko mwanamke. Mnapojadiliana nao kuhusu utunzaji katika ujauzito, jaribu kuwapa mapendekezo tendaji. Wanaume wanaojali sana afya ya wanawake walio katika maisha yao waweza kuwa hawajui pa kuanzia. Kwa mfano;

  • Mwelezee mwanamume kuwa mkewe aliye mjamzito anahitaji kusaidiwa katika kazi zake za kila siku (tazama Picha 2.4)
Picha 2.4 Wanawake wanahitaji usaidizi wa ziada katika kazi zao wakati wa ujauzito.
  • Wahimize wanandoa kupanga kwa pamoja mipango ya kuzaa na wawe na ufahamu wa dalili za hatari katika ujauzito, wakati wa kuzaa na baada ya kuzaa. Washauri waweke akiba ya pesa fulani ikiwa watapatwa na tukio la dharura na kupangia usafiri ikiwa mwanamke atahitajika kuenda kwenye kituo cha afya au hospitali.
  • Hakikisha kuwa mume anaelewa kuwa ni lazima akuite mkewe akipata uchungu (ikiwa ujauzito wake umekuwa wa kawaida na hana dalili zozote za hatari) ili uweze kuwa hapo anapozaa.
  • Hakikisha kuwa anajua mahali pa kumpeleka mkewe katika kituo cha afya kwa utunzaji wa dharura ikiwa matatizo yatatokea.
  • Muonyeshe jinsi mume anavyomsaidia mkewe wakati wa uchungu wa kuzaa. Kwa mfano wapi na jinsi ya kumsugua mgongo ili kutuliza maumivu yake.
  • Waambie wanaume jinsi wanavyoweza kupimwa na kutibiwa maambukizi ya zinaa kwa sababu ikiwa ni mwanamke tu atakayetibiwa, ataweza kuambukizwa tena na mwenzi wake kwa haraka.

2.3.2 Chagua mbinu za mawasiliano zitakazoifaa hadhira yako

2.3.4 Kuandaa kampeni ya afya