2.3.4 Kuandaa kampeni ya afya

Kampeni za kiafya hudumisha maarifa, ujuzi, mitazamo na maadili juu ya suala maalumu la kiafya. Pia zinaweza kutumika katika kutimiza mradi maalumu wa maendeleo ya jamii. Shughuli halisi za kampeni ya kijamii mara nyingi hufanyika kwa muda wa juma au mwezi mmoja. Kwa sababu hii, kampeni hizi mara nyingi huitwa‘Majuma ya Afya’.

Kampeni ya kiafya kwa kuendeleza matumizi ya huduma za utunzaji katika ujauzito inaweza kuandaliwa kutokana na suala au tatizo moja lililotambuliwa na wanajamii wenyewe. Kwa mfano, kueneza habari kuhusu manufaa ya huduma hizi kwa wanawake wajawazito kunaweza kuwa kampeni iliyopewa kipaumbele katika jamii ambapo kiwango cha matumizi ya huduma hizi kilikuwa chini. Ikiwa kuna kamati ya afya katika jamii hii, inafaa kushughulika katika kutambua masuala yanayopaswa kuandaliwa kampeni za kiafya na kupanga hatua inayofaa kuchukuliwa.

Picha 2.5 Nembo ya kampeni ya ‘Mwezi wa Umama Salama’ nchi mojawapo barani Afrika mwezi Januari mwaka wa 2010.

Kampeni za kiafya zinaweza pia kuendeshwa kitaifa. Kwa mfano, nchi mojawapo barani afarika kampeni iitwayo ‘Mwezi wa Umama Salama’ iliendeshwa mwezi Januari mwaka wa 2010. Lengo la kampeni hiyo lilikuwa ‘Hakuna mama anayepaswa kufariki wakati wa kuzaa’ (Picha 2.5).

Tatizo lililotambuliwa lilikuwa kiwango cha juu cha vifo vya kina mama na matatizo yanayohusiana na ujauzito na kuzaa. Wakati huo huo, kulikuwa na kiwango cha chini cha matumizi ya huduma za afya kwa kina mama kama vile utunzaji katika ujauzito, wanawake kuzaa kwa kuhudumiwa na mtaalamu wa uzazi, na upangaji uzazi. Katika mwezi huo wote, kampeni za utetezi na uhamasishaji wa umma ziliendeshwa kwa kutumia mbinu tofauti za mawasiliano zikiwemo posta, runinga na redio. Kulikuwa na majadiliano ya jopo na washika dau, viongozi wa kidini, wabunge na wengineo kuhusu uzito wa tatizo la afya ya kina mama na kushirikiana katika utekelezaji mwafaka wa utoaji wa huduma hizi. Kampeni juu ya kupanga uzazi na kupewa mawaidha kuhusu Virusi Vya Ukimwi (VVU) na kupimwa pia iliendeshwa katika mwezi huo.

2.3.3 Utetezi na uhamasishaji wa jamii

2.3.5 Hafla spesheli za jamii