2.3.5 Hafla spesheli za jamii

Kila jamii ina tamasha, maadhimisho na sherehe zake. Kwa mfano kuadhimisha majira spesheli ya mwaka kama vile wakati wa kupanda, kuvuna na Mwaka Mpya. Kuna tamasha na siku nyingi za kidini na siku za kukumbuka matukio ya kitaifa na mashujaa. Hafla zingine huwa za kujifurahisha na kutulia kama vile sherehe ya kahawa. Zingine huhitaji kufikiria sana na kutafakari kwa utulivu. Watu husherehekea kwa njia tofauti kulingana na tamaduni na kanuni za jamii hiyo. Jamii nzima hushiriki katika sherehe hizi bila kujali azma ya sherehe hizo. Hafla hizi zote zinaweza kuwa matukio mazuri kuwasilisha habari juu ya utunzaji katika ujauzito na kuendesha shuguli zinazoendeleza afya ya kina mama na watoto wazawa.

2.3.4 Kuandaa kampeni ya afya

2.3.6 Vikundi vya majadiliano