Muhtasari wa Kipindi cha 2 cha somo

Umejifunza katika Kipindi cha 2 cha somo kuwa:

  1. Azma kuu ya kuendeleza utumiaji wa utunzaji katika ujauzito ni kupunguza idadi ya vifo vya kina mama kabla, katika na muda mfupi baada ya kuzaa, vya watoto wazawa na matatizo.
  2. Utunzaji katika ujauzito ni fursa ya kuendeleza mazungumzo na wateja ili kuimarisha jumbe za afya ya kina mama kuhusu dalili za hatari katika ujauzito, kuzaa na muda baada ya kuzaa na kuhakikisha kila mmoja anajua ni wapi pa kutafuta utunzaji huo.
  3. Kuendeleza afya hujumlisha shughuli zozote zinazosababisha afya bora katika jamii au nchi. Pia inaweza kuhusisha vitendo vya watu binafsi, vikundi, mashirika, taasisi na serikali. Elimu ya kiafya, uchunguzi wa kiafya na uzuiaji wa magonjwa huchangia shughuli za kuendeleza afya.
  4. Elimu ya kiafya huwawezesha watu kuongezakudhibitina kuendeleza afya yao ya familia na jamii zao kwa vitendo na juhudi zao wenyewe. Huu ni mpango unaofululizwa kwa msingi wa shughuli zilizopangwa na kuratibiwa kwa kuzingatia tamaduni, mila, lugha na raslimali za hadhira.
  5. Utetezi na uhamasishaji wa jamii husaidia kupata na kudumisha ushiriki wa watu binafsi wa matabaka mbalimbali, vikundi na sekta zilizo katika viwango tofauti katika jamii kwa kutimiza lengo linalokusudiwa.
  6. Kuelimisha viongozi watoa maoni wenye ushawishi, viongozi wa kidini, waume na kina baba ili wawe watetezi na wenzi katika kuendeleza afya ya wanawake wakati wa ujauzito, uchungu wa kuzaa na kuzaa. Hii ni muhimu sana.
  7. Kampeni za kuendeleza afya, hafla za mafunzo, vikundi vya majadiliano na mawasiliano na watu binafsi hufaa kuandaliwa kwa makini na kutumia njia tofauti za mawasiliano na uwasilishaji itakavyofaa.
  8. Majadiliano ya kikundi ndiyo mbinu inayotumika sana kwa kupitisha elimu ya kiafya. Huhusisha mawasiliano ya kutoa na kupokea habari ambapo washiriki hupewa nafasi sawa za kuwasilisha maoni yao na kubadilishana waliyoyapitia na mawazo yao.
  9. Msingi wa elimu ya kiafya ya kibinafsi ni kujenga uaminifu na maelewano, kuwezesha uwazi baina ya washiriki, uhuru wa kubadilishana mawazo na majibu ya mara moja kwa utekelezaji wa maazimio.
  10. Mahali pazuri pa kuanzia ni kuisikiza hadhira yako. Ukisha fahamu yale wanayoyajua unaweza kuwasaidia kujenga elimu waliyo nayo. Ukisikiliza utajifunza kutoka kwa wale unaowaelimisha.
  11. Toa nafasi zitakazoifanya huduma ya utunzaji katika ujauzito kuwa mpango wa jamii kwa kuendeleza utambuzi wa matatizo na suluhisho, upangaji na utekelezaji wa vitendo vifaavyo na kutathmini matokeo.

2.4.4 Kuhitimisha hafla

Maswali ya kujitathmini ya Kipindi cha 2 cha somo