Malengo ya Somo la Kipindi cha 3

Baada ya kusoma katika Kipindi hiki, unapaswa uweze:

3.1 Kufafanua na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyochapishwa katika herufi nzito. (Maswali ya kujitathmini 3.1 na 3.2)

3.2 Kutambua na kueleza sehemu muhimu za kimsingi za anatomia ya Sehemu ya siri za nje za kike na viungo vya ndani vya uzazi. (Maswali ya kujitathmini 3.2, 3.3 na 3.4).

3.3 Kueleza majukumu ya viungo vikuu vya anatomia kwenye mfumo wa uzazi wa kike na umuhimu wao katika huduma ya ukunga. (Maswali ya kujitathmini 3.3 na 3.4)

Kipindi cha 3 Anatomia na Fiziolojia ya mfumo wa Uzazi wa Kike

3.1 Baadhi ya istilahi za kawaida katika anatomia na fiziolojia