3.1 Baadhi ya istilahi za kawaida katika anatomia na fiziolojia

Utakumbana na istilahi nyingi mpya katika kujifunza anatomia na fiziolojia kwa mara ya kwanza. Unaweza kuwa na ufahamu wa baadhi yao kutokana na somo lako la biolojia katika shule ya upili. Katika Kipindi hiki, tumejaribu kutumia istilahi rahisi iwezekanavyo ili kukusaidia kuelewa unachokisoma. Kufafanua nyingi za istilahi zinazotumika katika anatomia na fiziolojia ni zaidi ya Kipindi hiki, lakini kufafanua nyingi za istilahi muhimu zinazotumika katika huduma ya ukunga kutakusaidia kutimiza malengo ya somo la Kipindi hiki na Vipindi vya 4 hadi 6.

Istilahi zinazotumika katika anatomia ya binadamu mara nyingi ni zile zinazoonyesha mahali kilicho kiungo kimoja kwa kulinganisha na kingine au mwili wote (tazama Kisanduku3.1). Utakumbana na istilahi za mahali mara nyingi katika Moduli hii.

Kisanduku 3.1 Baadhi ya istilahi za kawaida za mahali zinazotumika katika anatomi

Juu ya

Chini ya

Ya mstari wa kati wa mwili (ya kati)

Pembeni mwa mstari wa kati wa mwili (pande, kingo, kando)

Mbele ya, kabla ya, mbeleni mwa

Nyuma au nyuma ya

Malengo ya Somo la Kipindi cha 3

3.2 Anatomia na fiziolojia ya viungo za uzazi za kike