3.2 Anatomia na fiziolojia ya viungo za uzazi za kike

Jukumu la wanawake katika uzazi ni changamani sana kuliko la wanaume:

  • Wanawake hutoa ova (mayai), zinazoweza kutungishwa na mbegu ya kiume.
  • Baada ya utungisho, wanawake pia hubeba na kulinda fetasi inayokua katika uterasi.
  • Baada ya kuzaa, matiti hutoa maziwa ya kumstawisha mtoto.

Kiasili, kila mmoja wetu ana hamu ya kujua jinsi tunavyokua katika uterasi za mama zetu, jinsi fetasi inavyokua katika miezi tisa ya ujauzito, jinsi inavyostawishwa na jinsi mzunguko wa hedhi unavyodhibitiwa. Ili kuelewa haya na maswali mengine husika kuhusu majukumu ya wanawake katika uzazi, unapaswa kujifunza kuhusu anatomia ya viungo vya uzazi vya kike na kuelewa fiziologia (jukumu) ya kila viungo.

Tunaanza na mahali pa kianatomia vilivyo viungo vya uzazi vya kike ukilinganisha na mfumo wa mkojo (figo na kibofu cha mkojo), mfumo wa utumbo na viungo vingine vya karibu katika kaviti ya Pelvisi, (tazama Jedwali 3.2 na Mchoro 3.1 hapa chini).

Jedwali 3.2 Kaviti katika mwili wa binadamu

Kaviti ni nafasi katika mwili wa binadamu iliyo na viungo, viowevu na viungo vingine. Kwa mfano, Kaviti ya fuvu ina ubongo, kaviti ya kifua ina mapafu na moyo, kaviti ya fumbatio ina tumbo, matumbo, ini, mafigo na viungo zinginezo, kaviti ya Pelvisi ina viungo vya uzazi na kibofu cha mkojo. Fahamu kuwa kaviti ya pelvisi ndiyo sehemu ya chini ya kaviti ya fumbatio na hakuna kizuizi baina yazo.

Mchoro 3.1 Sehemu nusu ya kaviti ya Pelvisi inayoonyesha viungo za uzazi wa kike, mwili ukitazama kushoto. Utajifunza zaidi kuhusu istilahi za anatomia zilizotambulishwa katika mchoro huu Kipindi hiki cha somo kinapoendelea.
  • Tazama kwa maakini, mchoro 3.1 kwa muda wa takribani dakika mbili ukuzingatia mahali vilivyo viungo vilivyotambulishwa. Chagua istilahi za mahali zilizo sahihi kutoka kwa Jedwali 3.1 kwa kuelezea mahali uterasi ilipo kwa kulinganisha na kibofu cha mkojo.

  • Kibofu cha mkojo kiko mbele ya uterasi, au unaweza kusema kuwa uterasi iko nyuma ya kibofu cha mkojo. Sehemu ya juu ya uterasi inainama juu ya kibofu hicho na iko juu yake au unaweza kusema kuwa kibofu cha mkojo kiko chini ya sehemu ya juu ya uterasi.

    Mwisho wa jibu

Nyuma ya uterasi, seviksi na uke katika mchoro 3.1, unaweza kuona sehemu ya koloni na rektamu ambapo uchafu mgumu huelekezwa nje ya mwili kupitia mkunduni. Kujua kuhusu mahali pa kianatomia vilivyo viungo hivi vyote ni muhimu sana katika ujauzito, leba na kuzaa. Kwa mfano, kwa mwanamke mjamzito, uterasi kuwa kubwa kutokana na fetasi inayokua itasukuma kibofu cha mkojo na koloni. Hii mara nyingi inaweza kusababisha kibofu kushindwa kudhibiti mkojo na hatimaye mwanamke huyo sharti akojoe mara nyingi zaidi na pia kufunga choo.

Unaposoma kuhusu mfumo wa uzazi wa kike, unafaa kujua kuwa viungo vyake vimegawanywa katika makundi mawili mapana. Viungo vilivyo nje ya uke vinasemekana kuwa Sehemu ya siri za nje za kike, ilhali vilivyo juu (ikiwa ni pamoja na mwanya wa uke) na ndani ya uke vinaitwa viungo za ndani za uzazi wa kike. Tayari umeona baadhi ya viungo katika makundi yote kwa kutazama kutoka upande mchoro 3.1. Sasa tutaangazia kila kundi kwa kina zaidi.

3.1 Baadhi ya istilahi za kawaida katika anatomia na fiziolojia

3.3 Sehemu ya siri ya nje ya uke