3.3 Sehemu ya siri ya nje ya uke

Tazama Picha 3.2 kwa makini. Viungo vyote vinavyoonekana kutoka nje, vinavyozunguka mianya ya urethra na uke, ikiwa ni pamoja na kinena, labia kubwa, labia ndogo, vestibuli na msamba, vinaunda Sehemu ya siri za nje za uke. Wakati mwingine viungo hivi kwa pamoja huitwa vulva.

Mchoro 3.2 Sehemu ya siri za nje za kike (au vulva).

Hamasa tofauti za hisi zinaweza kusababisha mwitikio kwenye neva zilizo katika viungo vya Sehemu ya siri za nje za kike kama vile mguso, maumivu, shinikizo na kiwangojoto. Hii huvifanya viungo hivi kuwa na hisia na kutiwa ashiki anapoguswa hasa na mwenzi wa kiume. Kufuatia haya, tendo la ngono kati ya mwanamume na mwanamke husababisha ushushaji wa manii kwenye viungo za uzazi za ndani za kike na kuanzisha mchakato wa utungisho, ujauzito, leba na kuzaa.

  • Tambua katika Mchoro 3.2 kuwa mwanya wa urethra, ​​wa uke na mkundu yote imekaribiana kwa pamoja kwenye vulva. Je, unafikiri uhusiano huu wa karibu una umuhimu gani wa kiafya kwa mwanamke mjamzito?

  • Jinsi ujuavyo, eneo karibu na mkundu huchafuliwa na bakteria kutoka kwa uchafu unaotoka kwenye ufereji wa utumbo. Kwa hivyo, maambukizi ya moja kwa moja ya vimelea vya bakteria kwenye mwanya wa urethra na uke hutokea kwa urahisi.

    Mwisho wa jibu

Ni muhimu sana kumshauri mwanamke mjamzito ahakikishe usafi kwenye eneo hili kwa kuzingatia usafi wa kibinafsi. Maambukizi kwenye kibofu cha mkojo na uke ni ya kawaida katika ujauzito, na ikiwa vimelea vya bakteria vitaingia katika uterasi yake, anaweza kumpoteza mtoto.

Sasa tutaangazia kila kiungo kilicho katika Mchoro 3.2, na tutaanza vile vilivyo kwenye kingo za nje, na kumalizia na vile vya kati.

3.2 Anatomia na fiziolojia ya viungo za uzazi za kike