3.3.1 Kinena

Kinena ni sehemu nene yenye mafuta na umbo la nusu mviringo iliyofunikwa na nywele. Sehemu hii iko juu ya kinena simfisisi. Simfisisi ni aina ya jointi thabiti isiyosogezeka na huwa kati ya mifupa. Jinsi utakavyoona katika Kipindi cha 6 cha somo (Mchoro 6.1), nusu mbili za mfupa wa kinena zimeunganishwa katikati na simfisisi ya kinena. Jukumu la tishu ya mafuta kwenye kinena ni kukinga eneo la kinena la mwanamke dhidi ya kuvilia anaposhiriki ngono.

3.3 Sehemu ya siri ya nje ya uke

3.3.2 Labia kubwa na labia ndogo