3.3.2 Labia kubwa na labia ndogo

Labia kubwa ni mapindo mawili marefu ya ngozi yenye mafuta na yaliyofunikwa na nywele. Mapindo haya hufunika na kulinda viungo zingine za Sehemu ya siri za nje za kike.

Labia ndogo ni mapindo mawili madogo ya tishu yaliyofunikwa na labia kubwa. Hulinda mwanya wa uke na urethra. Labia ndogo kwa kawaida ni nyumbufu kiasili, sifa inayoziwezesha kutanuka na kunywea wakati wa ngono, leba na kuzaa.

  • Je, unyumbufu huu husaidiaje wakati wa kuzaa?

  • Labia ndogo zinaweza kutanuka ili kuruhusu kichwa cha mtoto kitoke.

    Mwisho wa jibu

Katika nchi zingine, zikiwemo sehemu fulani za Afrika, labia ndogo na kisimi (kilichoelezewa hapa chini) zinaweza kuondolewa na ukeketaji ambao ni mojawapo ya desturi zenye madhara.

Ukeketaji umejadiliwa katika moduli juu ya Afya ya Uzazi wa vijana.