3.3.3 Vestibuli

Vestibuli ni eneo kati ya labia ndogo lililo na kisimi, mianya ya urethra na uke.

Kisimi ni viungo vifupi vyenye uwezo wa kudisa iliyo juu ya vestibuli. Viungo hivi vina neva na mishipa ya damu kwa wingi. Jukumu lake ni kumsisimua mtu wakati wa ngono na ni nyepesi sana kuhisi hasa kwa mguso. Mahali ilipo kianatomi ni sawa na mahali ulipo uume kwa mwanamume.

Ikiwa kisimi na labia ndogo zitaondolewa kwa ukeketaji, mwanya wa uke hautapanuka kwa urahisi wakati wa kuzaa kutokana na kuwepo kwa kovu mahali ambapo tishu iliondolewa. Hii inaweza kusababisha ugumu wakati wa leba na kuzaa, kukiwemo kuvuja damu nyingi na kupasuka kwa tishu iliyojeruhiwa. Wakati mwingine hali hii husababisha fistula - shimo kwenye ukuta wa uke.

  • Ukeketaji unaohusisha labia ndogo na kisimi kwa kawaida hutekelezwa bila dawa ya ganzi. Je, kutatokea athari zipi kwa mwanamke?

  • Kutakuwa na uchungu mwingi kutokana na kuwepo kwa neva kwenye eneo hili. Hali hii inaweza kusababisha kuzirai.

    Mwisho wa jibu.

Pia, labia ndogo na kisimi huwa na mishipa ya damu kwa wingi kwa hivyo kuzikata husababisha kutoka kwa damu nyingi, ambayo inaweza kusababisha kuzirai na mshtuko.

Mwanya wa urethra ndio mdomo au mwanya wa urethra. Ni kiungo chenye muundo wa neli ambacho hutoa mkojo kutoka kwenye kibofu cha mkojo. Katika Kipindi cha 22 mwishoni mwa Moduli hii, na katika madarasa yako ya mafunzo tendaji, utajifunza jinsi ya kuingiza neli ndogo iitwayo katheta kwenye mwanya huu ili kutoa mkojo kwenye kibofu. Hii inaweza kuwa ya muhimu wakati wa huduma ya dharura kwa mwanamke mjamzito, au wakati wa leba na kuzaa ikiwa hawezi kukojoa kivyake kwa sababu tishu za vestibuli zimevimba na kuibana urethra.

Mwanya wa uke ndio mlango wa ukeni. Hapa ndipo utakapoanza kuona sehemu ya mtoto inayotangulia kutoka mwanya huu unapopanuka na kufunguka leba unapodidimia.

3.3.2 Labia kubwa na labia ndogo

3.3.4 Msamba na kizinda