3.3.4 Msamba na kizinda

Eneo lenye misuli lililofunikwa na ngozi kati ya mwanya wa uke na mkundu huitwa msamba. Eneo hili lina misuli dhabiti na neva na husaidia kwa kuegemeza viungo vilivyo kwenye kaviti ya pelvisi. Kizinda ni pindo la tishu nyembamba ya uke na hufunika sehemu fulani ya mlango wa uke kwa wasichana. Inaweza kuraruka wakati wa mazoezi yanayohitaji nguvu nyingi na vile vile kushiriki ngono kwa mara ya kwanza.

3.4 Viungo vya ndani vya uzazi wa kike