3.4.1 Mishipa ya falopio na ovari

Anza kwa kuutazama kwa makini mchoro 3.3. Jinsi unavyoona katika mchoro, kuna mishipa ya falopio miwili, mmoja kila upande wa uterasi. Miisho ya mishipa hii, iliyo mithili ya vidole (iitwayo fimbriae), iko karibu na ovari kwa upande huo huo na hufunguka kuelekea kwenye kaviti ya pelvisi. Hii ina maana kuwa kukiwa na maambukizi kwenye kaviti ya pelvisi yanaweza kuingia kwenye uterasi kupitia mishipa ya falopio. Vile vile, kukiwa na maambukizi kwenye uterasi, yanaweza kuenea katika mishipa ya fallopio hadi kwenye kaviti ya pelvisi kisha kwenye fumbatio nzima huku yakiathiri viungo vingine. Haya yanaweza kuwa hatari yasipotibiwa mapema.

Mchoro 3.3 viungo vya viungo za ndani za uzazi wa kike

Ovari ni jozi ya viungo za uzazi wa kike ambazo hutoa mayai (ova). Viungo hizi huwa kwenye kaviti ya pelviksi, moja kila upande wa uterasi chini ya mianya ya mishipa ya fallopio (tazama Mchoro 3.3). Viungo hizi hukaa mahala pake kwa kujishikiza kwenye ligamenti mbili. Ligamenti ni tishu za kuunganisha zenye unyuzi na uwezo wa kupindika zinazoshikilia viungo mbalimbali vya ndani ya mwili. Pia huunganisha mfupa mmoja kwa mwingine katika jointi.

Wanawake huzaliwa wakiwa na idadi isiyobadilika ya takribani mayai (ova) 60, 000 yasiyopevuka. Mayai haya huwa katika vishimo vidogo kwenye ovari viitwavyo foliko za ovari. Kila ova ina uwezo wa kupevuka na kuwa tayari kwa utungisho lakini ni mayai 400 tu yanayopevuka wakati wa maisha ya mwanamke. Kila mwezi foliko kadhaa za ovari huanza kuwa kubwa na ova iliyo ndani kuanza kupevuka, lakini kwa kawaida, ni moja tu itakayoachiliwa kutoka kwenye ovari. Utoaji wa ova huitwa ovulesheni. Foliko zingine zilizosalia kuanyeusi.

  • Je, ni nini kinachoweza kutendeka iwapo ova mbili zitaachiliwa kwa wakati mmoja?

  • Mwanamke huyo anaweza kupata ujauzito wa mapacha.

    Mwisho wa jibu

Foliko za ovari zinazokua pia hutoa homoni za uzazi wa kike ambazo ni estrojeni na projesteroni ambazo ni muhimu kwa kudhibiti mzunguko wa hedhi kila mwezi na katika ujauzito. Utajifunza mengi zaidi kuhusu homoni hizi katika vikao vya 4 na 5 vya somo.

Homoni ni kemikali za kutuma ishara ambazo hutengenezwa mwilini na kuzunguka katika damu. Homoni tofauti hudhibiti shughuli za seli au viungo tofauti.

Baada ya ovulesheni sehemu ya ndani ya hiyo foliko tupu hukua na kutengeneza kitu chenye rangi ya manjano ndani ya ovari kiitwacho kopasi luteamu, ambayo hufanya kazi kwa muda kama viungo ya kutoa homoni.

Kopasi luteamu hutoa estrojeni na projesteroni kwa takribani siku 14 zitakazofuata. Estrojeni hunenepesha tishu-mafuta kwenye kuta za uterasi kukiwa na mimba. Projesteroni husimamisha ovulesheni zaidi wakati wa mimba.

  • Je, kwa nini ni muhimu kuzuia ovulesheni zaidi mara tu mwanamke anapokuwa mjamzito.

  • Hii ina maana kuwa mwanamke huyo hawezi kupata ujauzito mwingine akiwa tayari ujauzito huu ndiposa virutubishi vyake vyote viweze kutumika katika kustawisha na kukinga fetasi ya kwanza inayokua katika uterasi yake.

    Mwisho wa jibu

Ikiwa ujauzito haukutokea katika siku 14 baada ya ovulesheni, kopasi luteamu kua nyeusi na kuacha kutoa projestoreni. Matokeo ya haya ni kukatizwa kwa damu inayoletwa katika tishu-mafuta hizi za ziada kwenye kuta za uterasi na kusababisha kusawijika pia kwa tishu hizi za ziada na hatimaye kutolewa kupitia ukeni kama hedhi. Viwango vya estrojeni vinaweza kuanza kupanda na ovulesheni inaweza kutokea tena kwa mwanamke huyo mwezi unaofuata.

Ovari inapoachilia ova pevu (ovulesheni), fimbriae za mshipa wa falopio hugwia ova hiyo na kuielekeza kwenye uterasi. Mbegu ya kiume husonga kwenye mishipa ya falopio, hutungisha mimba ikutanapo na ova iliyoachiliwa (jinsi utakavyoona kwenye vikao vya 4 na 5 vya somo). Bitana ya Mishipa ya fallopio na vinyeso vyake hudumisha ova na manii, hurahisisha utungisho na hurutubisha ova iliyotungishwa hadi itakapofika kwenye uterasi.

3.4 Viungo vya ndani vya uzazi wa kike

3.4.2 Uterasi