3.4.2 Uterasi

Uterasi ni viungo wazi yenye misuli ambamo ova iliyotungishwa hupandikizwa na kukua kuwa fetasi. Jukumu kuu la uterasi ni kukinga na kurutubisha fetasi hadi itakapozaliwa.

Wakati wa ujauzito, kuta za uterasi zenye misuli hunenepa na kunyumbuka ili kuhimili fetasi inayokua wakati wa ujauzito. Pia ni lazima uterasi iweze kuhifadhi kioevu zaidi cha amnioni (maji yanayozingira fetasi kwenye mfuko wa membreni za fetasi) na kondo (kiungo kinachopeleka virutubishi kutoka kwa mama hadi kwa fetasi). Utajifunza mengi zaidi kuhusu haya katika Kipindi cha 5 cha somo.

  • Je, unafikiri ni kwa nini kuta zenye misuli za uterasi hunenepa wakati wa ujauzito?

  • Rusu nene ya misuli ina nguvu za kuhimili fetasi inayokua na vitu vingine vilivyo kwenye uterasi ambavyo huendelea kuwa vizito ujauzito unapozidi kukua.

    Mwisho wa jibu

Uterasi ina sehemu nne za kianatomia zilizoonyeshwa katika Mchoro 3.4:

  • Mwili: Ndiyo sehemu kuu ambayo iko upande wa juu na ni theluthi mbili za uterasi nzima.
  • Fandasi: sehemu juu ya uterasi iliyotanuka na iko katikati ya mwungano wa mishipa ya falopio.
  • Kaviti ya endometria: hii ni nafasi yenye umbo la pembe tatu katikati ya kuta za uterasi.
  • Seviksi: ni shingo nyembamba iliyo mwisho wa upande wa juu wa uke.
Mchoro 3.4 Muundo wa uterasi tupu ukionyesha hizo sehemu nne kuu.

Ukuta wa uterasi una rusu tatu za tishu, mbili nazo zimeonyeshwa katika mchoro 3.4:

  • Perimetriumu: hii ni rusu ya nje kabisa iliyoundwa kwa membreni nyembamba na hufunika uterasi. (Si muhimu kwako kujua istilahi hii kwa mujibu wa utunzaji wa ukunga)
  • Miometriamu: hii ni rusu ya katikati ambayo ni nene na yenye misuli ilivyoonyeshwa katika mchoro 3.4.
  • Endometriamu: hii ndiyo rusu ya ndani kabisa ya uterasi ambayo ni nyembamba na hunenepa wakati wa mzunguko wa hedhi. Hii ndiyo tishu inayokua na kujilimbikiza kila mwezi kwa mwanamke aliye katika umri wa uzazi kutokana na athari za homoni za uzazi za kike.
  • Je, ni nini kinachofanyika kwa endometriamu homoni zikiacha kuzunguka baada ya ovulesheni?

  • Kuletwa kwa damu hukatizwa na endometriamu kusawijika na kutolewa mwilini kupitia ukeni kama hedhi ya kila mwezi.

    Mwisho wa jibu

3.4.1 Mishipa ya falopio na ovari

3.4.3 Seviksi na uke