3.4.3 Seviksi na uke

Seviksi ni shingo nyembamba ya upande wa chini wa uterasi inayotengeneza kijia chenye umbo la neli kinachoelekea katika upande wa juu wa uke(tazama Mchoro 3.4). kwa kawaida huwa na urefu wa takribani centimita 3 hadi 4.

Uke ni kijia chenye misuli, na urefu wa takribani centimita 8 hadi 10 kilicho kati ya seviksi na viungo vya uzazi vya nje. vioevu vinavyolainisha uke hutoka kwenye tezi zilizo katika sevikisi.

  • Uke una majukumu matatu. Je, unaweza kuyataja?

  • Ndiyo viungo inayoupokea uume wakati wa kushiriki ngono na ndipo manii yanapowekwa. Ndio njia ambapo hedhi hutokea kila mwezi kwa mwanamke asiyepata ujauzito. Pia ndiyo njia ambapo mtoto hupitia anapozaliwa.

    Mwisho wa jibu

Wanawake wajawazito wanapaswa kuhimizwa kutia nguvu misuli ya uke kwa kuibana kwa ukakamavu wanavyoweza kwa angalau mara kumi na kurudia zoezi hili kwa angalau mara nne kila siku. Mwanamke anaweza kujifunza jinsi ya kulifanya zoezi hili anapokojoa. Mwanamke anapaswa kuibana misuli ya uke anapokojoa, mkojo usimame, kisha ailegeze misuli hiyo mkojo utiririke tena. Mara tu anapojua jinsi ya kuibana misuli hii, anapaswa kulifanya tu zoezi hili wakati hakojoi. Kufanya zoezi hili la kubana kunaweza kusaidia katika:

  • Kuzuia kuvuja kwa mkojo
  • Kuzuia kuraruka kwa uke na msamba viungo hivi vinapotanuliwa wakati wa kuzaa
  • Kuharakisha uponaji baada ya kuzaa
  • Kuongeza furaha ya ngono

Katika Kipindi hiki umejifunza viungo na majukumu ya viungo katika mfumo wa uzazi wa kike na umuhimu wao katika utunzaji wa ukunga. Katika Kipindi kitakachofuata utaangazia udhibiti wa homoni kwa mzunguko wa uzazi kwa wanawake.

Muhtasari wa Kipindi cha 3