Muhtasari wa Kipindi cha 3

Katika Kipindi cha 3 umejifunza kuwa;

  1. Anatomia ni somo juu ya viungo vya mwili wa binadamu na fiziolojia ni somo juu ya majukumu patanifu ya viungo, tishu na mifumo ya mwili.
  2. Mfumo wa uzazi wa kike umegawanywa katika sehemu ya ndani ya genitalia (chini na nje ya mwanya wa uke) na viungo vya uzazi vya ndani (juu ya mwanya wa uke katika kaviti ya pelvisi)
  3. Viungo vya uzazi vya ndani viko karibu na kibofu, utumbo mkubwa na rektamu; mwanya wa nje wa uke uko karibu na ule wa urethra na mkundu. Uhusiano huu wa karibu huongeza uwezekano wa kuenea kwa maambukizi katika eneo la genitalia.
  4. Katika jamii zingine za kitamaduni, kisimi na labia ndogo mara nyingi huondolewa kwa ukeketaji; hii inaweza kusababisha athari za hatari kubwa (hata zinazoweza kusababisha kifo) kwa mwanamke huyo, hasa wakati wa leba na katika kuzaa.
  5. Ovari ni viungo za uzazi vya kike ambavyo hutoa ova moja kila mwezi katika miaka ya uzazi. Mmoja wa mishipa ya falopio hubeba ova kutoka kwa ovari hadi kwenye uterasi. Utungisho hufanyika katika mshipa wa falopio.
  6. Uterasi ni viungo vyenye misuli inayoipa fetasi inayokua ulinzi na chakula wakati wa ujauzito.
  7. Homoni za uzazi wa kike; estrogeni na projesteroni huelekeza upevukaji wa ova kwenye ovari, utoaji wa ova (ovulesheni) na unenepaji wa endometria (bitana yenye mafuta kutani mwa uterasi). Endometriamu hukwangulika na kutolewa kama hedhi ikiwa utungisho na ujauzito hautatokea.
  8. Uke ndiyo kiungo inayoupokea uume wakati wa kushiriki ngono. Ndiyo njia ambapo hedhi hutokea, na pia hutengeneza sehemu ya chini ya njia ya uzazi.

3.4.3 Seviksi na uke

Maswali ya kujitathmini ya Kipindi cha 3