Maswali ya kujitathmini ya Kipindi cha 3

Kwa kuwa umekamilisha Kipindi hiki, unaweza kutathmini ni kwa kiwango kipi umeweza kutimiza malengo yake kwa kujibu maswali haya. Yaandike majibu yako katika daftari lako na uyajadili na Mkufunzi wako katika Kipindi Kitakachofuata cha Masoma ya Kusaidiana. Unaweza kuyalinganisha majibu yako na muhtasari juu ya Maswali ya Kujitathmini mwishoni mwa Moduli hii.

Swali la kujitathmini 3.1(linatathmini Malengo ya Somo 3.1 na 3.2)

Tazama mchoro 3.5. Andika majina ya viungo vya mwili vilivyopachikwa herufi ‘a’ hadi ‘i’.

Mchoro 3.5.Andika majina ya viungo vya ndani vya uzazi wa kike ili kukamilisha maswali ya kujitathmini 3.1.

Answer

Majibu sahihi ya majina kwa mchoro 3.5 ni kama ifuatavyo:

  • a.ni uke
  • b.ni seviksi
  • c.ni uterasi
  • d.ni ovari
  • e.ni fandasi
  • f. ni ligamenti inayoshikilia ovari
  • g.ni mshipa wa falopio
  • h.ni fimbriae
  • i.ni ligamenti ya ovari

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 3.2 (linatathmini Malengo ya Somo 3.1)

Chagua istilahi sahihi za sehemu kutoka katika jedwali 3.1 kueleza mahali panaporejelea zilipo uterasi na rectamu katika mcharo 3.1.

Answer

Uterasi iko mbele na juu ya rektamu. Njia nyingine ya kueleza sehemu hizi ni kusema kuwa rektamu iko nyuma na chini ya uterasi.

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 3.3 (linatathmini Malengo ya Somo 3.2 na 3.3)

Je, ni viungo vipi vinavyoondolewa kwa ukereketaji na ni madhara yapi yanayoweza kumkumba mwanamke wakati wa leba na katika kuzaa?

Answer

Viungo vinavyoondolewa kwa ukereketaji ni kisimi na labia ndogo. Kovu inayotokea mikato inapoendelea kupona huzuia uwezo wa kawaida wa vulva kutanuka wakati wa kuzaa ili kuruhusu mtoto kupita kwenye njia ya uzazi. Kutokana na haya, kuzaa kunaweza kuzuiliwa kisha uke uraruke na kusababisha maumivu makali na upotezaji wa damu. Wakati mwingine nasuri (shimo kwenye ukuta wa uke) inaweza kuraruka na upotezaji wa damu unaweza kuhatarisha maisha ya mwanamke huyo.

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 3.4 (linatathmini Malengo ya Somo 3.2 na 3.3)

Je, ni kauli ipi kati ya hizi isiyo kweli? Taja ni kwa nini kauli hiyo si kweli.

  • A.Maambukizi katika uterasi yanaweza kuingia kwenye kaviti ya pelvisi kupitia ukeni.
  • B.Msamba ni sehemu yenye misuli katikati ya mwanya wa uke na mkundu.
  • C.Upevukaji wa ova hudhibitiwa na homoni za uzazi wa kike.
  • D.Tezi zilizo kwenye seviksi hutoa vinyeso vinavyolainisha uke.
  • E.Fandasi ndiyo ‘shingo’ nyembamba iliyo kwenye upande wa chini wa uterasi.

Answer

  • A.Si kweli. Maambukizi kwenye uterasi yanaweza kuingia katika kaviti ya pelvisi kupitia katika mishipa ya falopio ambayo iko wazi upande wa mwisho. Maambukizi katika uterasi yanaweza kuenea ukeni na mara nyingi hujitokeza kama mchozo unaonuka kutoka kwenye mwanya wa uke katika vulva.
  • B.Ni kweli. Msamba ni sehemu yenye misuli katikati ya mwanya wa uke na mkundu.
  • C.Ni kweli. Upevukaji wa ova hudhibitiwa na homoni za uzazi wa kike.
  • D.Ni ukweli. Tezi zilizo kwenye seviksi hutoa unyeso unaolainisha uke.
  • E.Si kweli. Fandasi ndilo jina inayopewa sehemu yenye umbo la kuba juu ya uterasi. Shingo nyembamba kwenye sehemu ya chini ya uterasi huitwa seviksi.

Mwisho wa jibu.

Muhtasari wa Kipindi cha 3