4.2 Mzunguko katika ovari

Mzunguko katika ovari ni mfuatano wa shughuli za kila mwezi zinazohusiana na upevukaji na uachiliaji wa ova, maandalizi ya utungisho na pandikizo kwenye uterasi (ikiwa kutatokea utungisho). Unaweza kuwa unashangaa ni kwa nini udhibiti wa mfumo wa uzazi wa kike ni changamano jinsi ilivyoonyeshwa katika mchoro 4.1. Sababu ni kuwa mzunguka katika ovari sharti uanzishwe kisha usitishwe kwa utaratibu uliodhibitiwa sawasawa kila mwezi. Katika sehemu hii tutaeleza jinsi haya yanavyotimizwa.

Mzunguko katika ovari huwa katika awamu mbili zinazofuatana. Kila awamu huchukua muda wa takribani siku 14. Matukio hubainishwa kutoka siku ya 1 ambayo ndiyo siku ya kwanza ya kipindi cha mwisho cha kawaida cha hedhi.

4.1 Homoni za uzazi wa kike

4.2.1. Awamu ya foliko: siku ya 1 hadi ya 14