4.2.1. Awamu ya foliko: siku ya 1 hadi ya 14

Mfuatano ulioonyeshwa katika mchoro 4.1 umeanza na hipothalamasi kutoa homoni itoayo gonadotropini, ambayo huichochea tezi ya pituitari kutoa Homoni Chochelezi ya Foliko (HCF) na homoni ya lutea ambazo kisha huiathiri ovari kwa kuzifanya foliko za ovari kuhitimisha upevukaji wa ova. Katika kipindi hiki, foliko chache za ovari zilizo na ova zisizopevu hukua na kupevuka kutokana na uchochelezi wa Homoni Chochelezi ya Foliko na homoni ya lutea. Kwa kawaida, kufikia siku ya 14, ni foliko moja tu ambayo huwa pevu na tayari kuitoa ova iliyo ndani yake. Foliko zingine zote zilizokuwa zimeanza kupevuka katika awamu hii ya mzunguko wa ovari kua nyeusi mara tu baada ya ovulesheni.

Fahamu kuwa ni kipindi kimoja tu kisichobadilika kwa kiasi kwa wanawake wote, nacho ni muda kati ya ovulesheni na mwanzo wa hedhi ambacho ni sawa kwa wanawake wote na huchukua kwa kawaida karibu siku 14 hadi 15. Hata hivyo wakati wa ovulesheni hubadilika na ni vigumu kuubashiri kwa usahihi.

4.2 Mzunguko katika ovari

4.2.2 Awamu ya lutea: siku ya 15 hadi ya 28