4.3.1 Awamu ya hedhi; siku ya 1 hadi ya 5

Ikiwa utungisho haukutendeka baada ya ovulesheni, kopasi leteamu itasawijika na utoaji wa projesteroni kupungua na hatimaye kichochelezi kinachoidumisha endometriamu nene kupotea. kupunguka kwa kiwango cha projesteroni husababisha kukwangulika kwa bitana nene ya endometriamu. Ukuta wenye misuli wa uterasi (miometriamu) hunywea ili kusaidia kukatiza kuletwa kwa damu kwenye endometriamu na kuifanya kujitenga kutoka kwa uterasi. Endometriamu inapochanguka na kutokea ukeni huwa imechanganyika na damu kiasi kwa sababu awali ilikuwa na mishipa mingi ya damu kwa ustawishaji wa fetasi iwapo kungetokea ujauzito. Mchanganyiko wa tishu na damu hutolewa kupitia ukeni kama kioevu cha hedhi kwa kawaida kwa muda wa takribani siku 3 hadi 5. Majina mengine ya hedhi ni kutokwa na damu kila mwezi au kipindi cha hedhi.

Hedhi hutoka kila mwezi kwa muda wote wa miaka ya uzazi isipokuwa wakati wa ujauzito ampapo husitishwa na mwanamke hawezi kupata ujauzito mwingine hadi mtoto atakapozaliwa. Unyonyeshaji wa mtoto pia husitisha hedhi bali kunayo hatari kwamba ovulesheni na ujauzito vinaweza kutokea.

4.3 Mzunguko katika uterasi

4.3.2 Awamu ya kuongezeka: siku ya 6 hadi ya 14