5.1.1 Mbegu za uzazi za kiume: seli za uzazi za kiume

Seli ya mbegu ya kiume iliyokomaa (tazama Mchoro 5.1) ni seli ndogo ya kizazi ya kiume inayoogelea. Seli hii ina kichwa, mwili na mkia. Kichwa chake kimefunikwa na chepeo na kina kiiniseli cha chembe nzito za kijenetiki. Kichwa hiki kimeshikishwa kwenye sehemu iliyo na mitokondria, ambayo husambaza nguvu za kuiwezesha mbegu hii kutenda kazi. Mkia wa mbegu hii unaweza kukunjika na kunyooka, hivyo kuifanya isonge kwa mwendo kama wa wimbi.

Mchoro 5.1 Muundo wa mbegu za uzazi za kiume (seli ya uzazi ya kiume)
  • Tazama Mchoro 5.1. Je, unaweza kueleza jinsi mbegu ya uzazi ya kiume inavyosonga ukeni, uterasini, na kisha kwenye mishipa ya falopio?

  • Mkia wa mbegu ya kiume hujipinda kutoka upande hadi mwingine, hivyo kuisongesha mbele. Mitokondria ni oganeli zinazotolesha nguvu katika seli. Oganeli hizi husambaza nguvu kwenye mkia wa mbegu ya kiume ili kuiwezesha kusonga.

    Mwisho wa jibu.

Mbegu ya kiume hujumuisha takriban 5% pekee ya manii yanayotolewa na mwanaume wakati wa ngono. Takriban mbegu milioni 100 - 400 hutolewa kila wakati. Mbegu hizi hubebwa kwenye kiowevu kilicho na virutubishi (manii), kinachosaidia kuziweka hai. Mbegu za kiume ni ndogo sana. Mbegu moja ndiyo seli ndogo zaidi katika mwili wa mwanamume.

Mbegu mpya hukua katika kende (korodani) kuanzia kipindi cha kubaleghe hadi utu uzima wa mwanaume. Mbegu hukua hadi kupevuka kwa takriban siku 72. Kutoleshwa kwa mbegu za kiume huhitaji kiwangojoto cha mwili cha nyusi 3 – 5 chini ya kile cha kawaida. Hii ndiyo sababu makende huwa nje ya fumbatio. Makende yanapofikiwa na kiasi kingi cha joto, uzalishaji wa mbegu unaweza kutatizika na kusababisha ugumba.

5.1 Seli za uzazi za kiume na za kike

5.1.2 Ova: mbegu za kizazi za kike