5.1.2 Ova: mbegu za kizazi za kike

Kama ulivyojifunza katika Kipindi cha 3, mtoto wa kike huzaliwa akiwa na ova zote atakazokuwa nazo maishani mwake, ingawa zikiwa bado hazijapevuka. Kila ova ni seli kubwa yenye membreni iliyo nje. Ova huwa imejaa kiowevu chenye wingi wa protini. Ova ina kiiniseli chenye chembe za kijenetiki za kike.

Ova huhifadhiwa kwenye foliko za ovari, na ova chache huanza kupevuka kila mwezi baada ya msichana kubaleghe afikiapo umri wa takriban miaka 12 -15. Utaratibu huu huendelea hadi wakati wa ukomohedhi, afikiapo takriban miaka 48 - 50, wakati ambapo vipindi vya hedhi hukoma.

  • Ni homoni zipi zinazosisimua ova ili kuiwezesha kupevuka?

  • Haipothalamasi iliyo ubongoni hutolesha homoni inayotoa gonadotropini (GnRH). Homonihii husisimua tezi ya pitituari (iliyo ubongoni pia) ili kutolesha homoni ya kusisimua foliki (HKF) na homoni ya lutea (HL). Homoni hizi mbili hutenda kazi kwa pamoja kwenye foliki za ovari na kusababisha baadhi ya foliki hizi kuanza kupevuka.

    Mwisho wa jibu

  • Ikiwa siku ya kwanza ya hedhi inaitwa Siku ya 1 ovari itaachilia ova iliyopevuka baada ya siku ngapi (ovulesheni)?

  • Kwa wanawake wengi, ovulesheni hufanyika takriban siku ya 14 baada ya hedhi.

    Mwisho wa jibu.

5.1.1 Mbegu za uzazi za kiume: seli za uzazi za kiume

5.2 Utungisho