5.2 Utungisho

Utungisho ni kuunganika kwa kiiniseli cha mbegu za uzazi za kiume na kiiniseli cha ova. Ili utungisho utokee, ni sharti mbegu za kiume ziingie ukeni katika kipindi kisichozidi siku 3 kabla ya ovulesheni au katika kipindi kisichozidi siku moja baada ya ovulesheni. Kipindi cha ovulesheni ni kifupi kwa sababu mbegu za kiume na ova huishi kwa muda mfupi, na zote hufa zisipokutana na kuungana katika kipindi hiki. Kufuatia ovulesheni, ova huchukuliwa na fimbria ya mshipa wa falopio iliyo katika upande huo wa mwili ambapo ovari iliachilia ova. Ova hubaki kwenye mshipa wa falopio ikiwa ingali hai na inayotenda kazi vyema kwa muda wa saa 12 - 24. Mbegu za kiume zinaweza kuishi kwa muda mrefu zaidi kwenye mfumo wa uzazi wa mwanamke, kwa takriban saa 72, ingawa nyingi hufa mapema.

Mbegu za kiume ziingiapo ukeni huogelea kupitia katika seviksi huku zikiingia kwenye uterasi, kisha kuingia kwenye mishipa ya falopio. (Tazama tena Mchoro 3.3.) Utungisho wa ova hufanyika katika mshipa wa falopio. Kukazana kwa misuli ya kuta za uterasi na mishipa ya falopio husaidia kusongesha mbegu za kiume. Mbegu hizi zinaweza kuogelea milimita kadhaa kwa sekunde, hivyo zinaweza kufika katika mishipa ya falopio kwa muda wa takriban dakika 15. Hata hivyo mamilioni ya mbegu hizi hufa zikiwa zingali zinasonga.

Mchoro 5.2 Utungisho wa ova ya binadamu.

Mbegu moja tu kiume ndiyo hufaulu kutungisha ova (Mchoro 5.2) kwa kupenyeza hadi ndani ya membreni ya seli na kuwekeza chembe za kijenetiki za kiume kwenye seli ya kike, ambapo viiniseli hivi viwili huungana. Ova iliyotungishwa (zigoti) punde hupinga kupenyeza kwa mbegu nyingine. Baada ya utungisho, zigoti hubaki kwenye msipa wa falopio kwa takriban saa 72. Zigoti hii hukua upesi katika kipindi hiki.

5.1.2 Ova: mbegu za kizazi za kike

5.3 Vipindi vya kwanza vya kukua kwa embrio