5.3 Vipindi vya kwanza vya kukua kwa embrio
Kuanzia utungisho hadi miezi 8 ya ujauzito, mwanadamu anayekua huitwa embrio. Kwanza, embrio hugawanyika na kuwa seli mbili. Seli hizi hugawanyika tena na kuwa seli nne (tazama Mchoro 5.3). Seli hizi hugawanyika mara nyingi hadi mviringo wa seli uitwao morula kujitokeza baada ya siku tatu. Seli zilizo katika morula zinapoendelea kugawanyika, huanza kusongea pembeni mwa mviringo huu hadi mwanya kufanyika. Mviringo huu huitwa blastosisti katika takriban siku tano baada ya utungisho. Fahamu katika Mchoro 5.3 kuwa blastosisti ina bonge la seli kwenye sehemu moja ya mwanya.
Embrio ya kwanza husongea kwenye mshipa wa falopio kuelekea uterasini pindi inavyoendelea kubadilika. Utaratibu huu huchukua muda wa siku 5 - 7
5.2 Utungisho