5.3.1 Upandikizaji

Siku 5 -7 baada ya utungisho, blastosisti hufika uterasini na kujishikisha kwenye endometriamu ilionenepa (sehemu ya ndani ya uterasi). Utaratibu huu hujulikana kama upandikizaji. Iwapo embrio itaendelea kuishi, kipindi cha ujauzito huanza. Hata hivyo, embrio huenda isijipandikize, au isidumu kwa siku nyingi. Ikiwa ni hivyo, embrio hutolewa uterasini huku endometriamu ikimenyeka, kisha kupitia ukeni kama damu ya hedhi. Mara nyingi, mimba ya siku chache huharibikia namna hii. Mwanamke anaweza kukosa kufahamu kuwa alikuwa mjamzito kwa kipindi kidogo.

Unapokisia kuwa mwanamke ana mimba ya kiektopi, mpe rufaa mara moja kwa...?

Mara kwa mara, upandikizaji hutokea kwenye mshipa wa falopio. Aina hii ya mimba, na ambayo ni hatari sana, huitwa mimba ya kiektopi. Embrio inapoendelea kukua, mshipa wa falopio unaweza kupasuka na kusababisha maumivu makali na damu kuvujia kwenye njia ya fumbatio.

Ikiwa blastosisti itafaulu kujipandikiza kwenye uterasi, seli huendelea kujigawa huku ikisongea kwenye sehemu mpya na kuchukua miundo miwili tofauti.

  • Seli tatu au nne za blastosisti hukua na kuunda sehemu ya ndani ya bonge la seli. Wiki chache baadaye, bonge hili huundika kuwa miundo maalum ya embrio ya binadamu iliyo na kichwa, moyo unaodunda na miguu na mikono midogo. Baadhi ya seli hizi pia hukua na kuwa membreni za fetasi, ambazo huunda mfuko wa maji uliozunguka embrio ili kuikinga.
  • Takriban seli 100 za blastosisti zinazosalia kutoka huunda trofoblasti ( hutengeneza trophoblasti ambayo huchangia kukua kwa plasenta ya mtoto). Awamu ya kwanza ya kukua kwa plasenta ni wakati seli za trofoblasti zinapoingia kwenye endometriamu.

Jedwali 5.1 linaeleza kwa muhtasari awamu muhimu za utaratibu wa kukua kwa binadamu kutoka utungisho hadi mwaka mmoja baada ya kuzaliwa.

Kisanduku 5.1 Awamu za kukua kwa binadamu baada ya utungisho

Utungisho: kuungana kwa ova na mbegu ya kiume katika siku ya kwanza

Morula: bonge la seli baada ya siku tatu

Blastosisti: bonge la seli lenye uwazi baada ya siku tano.

Trofoblasti: hutumika kuunda embrio katika vipindi vya kwanza, membreni ya fetasi na plasenta baada ya siku 5 -7.

Embrio: binadamu anayekua, kuanzia utungisho hadi wiki 8 za ujauzito.

Fetasi: Binadamu anayekua kuanzia wiki ya 9 ya ujauzito hadi kuzaliwa, baada ya wiki 40.

Mtoto mzawa: mtoto aliyezaliwa, kutoka siku ya kuzaliwa hadi siku 28.

Mtoto mchanga: mtoto aliye na umri chini ya mwaka mmoja.

5.3 Vipindi vya kwanza vya kukua kwa embrio