5.4 Plasenta

Plasenta ni kiungo cha muda mfupi kinachohitajika wakati embrio na fetasi inapokua. Plasenta husaidia katika ubadilishanaji wa virutubishi na oksijeni baina ya mama na fetasi, na kusafirisha takamwili za fetasi hadi katika mwili wa mama ili ziondolowe na viungo vya mwili vya mama. Damu ya mama na ya mtoto haichanganyiki katika plasenta. Katika kipindi hiki, utajifunza kuhusu jinsi damu huzunguka kwenye fetasi na plasenta na jinsi fetasi hulishwa na kuondoa kinyesi chake. Mfumo wa damu katika plasenta pia hukinga fetasi kutokana na kemikali na viini vya maambukizi vilivyo katika damu ya mama.

Kama ilivyoelezewa hapo juu, plasenta huanza kukua kutoka trofoblasti baada ya embrio kujipandikiza kwenye uterasi. Plasenta hukua kikamilifu katika kipindi cha miezi 2, kisha kuendelea kukua hadi leba inapoanza. Ifikapo wakati wa mtoto kuzaliwa, plasenta huwa na uzito wa kadri gramu 600.

5.4.1 Mishipa ya damu ya mama na mtoto