5.4.2 Mzunguko wa damu kwenye plasenta

Wakati wa kukua kwa fetasi, sehemu za plasenta huchomoza kwenye endometriamu ya mama. Michomozo hii midogo huitwa vili. Vili hutoa kemikali zinazomeng’enya, kuvunjavunja na kufungua kuta za ateri za mama kwenye endometiriamu, na kupelekea mianya kwenye endometiriamu kujaa damu yenye oksijeni na virutubishi kutoka kwenye ateri za endometiriamu za mama.

Hata hivyo, vidimbwi vya damu ya mama vilivyo kwenye plasenta havichanganyiki na damu ya fetasi. Kuta za ateri na vena ndogo zaidi (kapilari) zilizo katika plasenta hubakia nzima (hazimeng’enywi). Kapilari hizi hulowa kwa nje na damu ya mama, iliyotenganishwa na damu ya fetasi iliyo ndani ya kapilari na kuta za mishipa (Mchoro 5.5).

Mchoro 5.5 Mzunguko wa damu katika plasenta, unaoonyesha kapilari za fetasi zikiwa zimelowa damu ya mama.

Kapilari za fetasi katika plasenta zipo karibu sana na “dimbwi” la damu ya mama, iliyo na wingi wa oksijeni na virutubishi vilivyoyeyushwa, kuliko damu ya fetasi iliyo ndani ya mishipa ya fetasi.

  • Nini hutendetekea oksijeni na virutubishi vilivyo ndani ya damu ya mama katika hali hii?

  • Oksijeni na virutubishi huvuka kutoka ndani ya damu ya mama hadi katika damu ya fetasi kupitia kuta za kapilari. Utaratibu huu huitwa msambao. Kupitia utaratibu huu, mfumo wa mzunguko wa damu wa fetasi hupata oksijeni na virutubishi.

    Mwisho wa jibu.

  • Je, unafikiri takamwili zilizoyeyushiwa ndani ya damu ya fetasi hutolewa vipi zinapopitia kwenye plasenta?

  • Takamwili zilizoyeyushiwa ndani ya damu ya fetasi zinazoingia katika plasenta husambaa kupitia kuta za mishipa ya damu ya fetasi hadi katika damu ya mama. Damu ya mama kisha huzisafirisha taka hizi ili ziondolewe na maini na figo za mama.

    Mwisho wa jibu.

Plasenta ina sehemu kubwa inayosaidia kusafirisha dutu katika pande zote kupitia msambao, kama ilivyoelezwa hapo juu. Fahamu kwamba damu ya mama kamwe haichanganyiki na ya fetasi, bali huwa imetenganishwa kwa kuta za mishipa ya damu ya fetasi.

5.4.1 Mishipa ya damu ya mama na mtoto

5.4.3 Plasenta kama kichungi